
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari hatimaye ametangaza wizara na mawaziri watakaozisimamia, miezi saba baada yake kushinda uchaguzi wa urais.
Jenerali mstaafu Mansur Dan Ali atakuwa Waziri wa Ulinzi, na kazi yake kuu itakuwa kuongoza vita dhidi ya wanamgambo wa Boko Haram.
Gavana wa zamani wa jimbo la Lagos Babatunde Fashola ameteuliwa waziri wa kawi, ujenzi na makazi na anakabiliwa na kibarua cha kutatua mzozo wa umeme Nigeria.
Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mkulima Audu Ogbe ameteuliwa waziri wa kilimo.
Nigeria ina ardhi kubwa ambayo ikutumiwa vyema inaweza kubuni nafasi za kazi na kupunguza utegemezi wa mafuta, wadadisi wanasema.
Kuzinduliwa kwa baraza hilo lenye mawaziri 36 kumefanyika miezi saba baada ya uchaguzi wa urais.

biashara na uwekezaji, angeteuliwa waziri wa fedha.
Rais Buhari pia ameshangaza wengi kwa kumteua mkuu wa zamani wa jeshi Jenerali Abdurrahman Dambazau kuwa waziri wa mambo ya ndani. Wengi walitarajia angeteuliwa waziri wa ulinzi.
Amina Mohammed, mshauri wa zamani wa mkuu UN Ban Ki-Moon kuhusu maendeleo endelevu, alitarajiwa kuteuliwa waziri wa mipango lakini ameteuliwa waziri wa mazingira.