Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

MKAZI WA KIBENA NJOMBE APIGWA NA KUJERUHIWA KWA KUCHANA MABANGO YA DOKTA MAGUFULI

$
0
0

Yuda James Mkazi wa Kibena Anayedaiwa Kupigwa na Kujeruhiwa Mkono na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wakiongozwa na Erasto Ngole Jana.

Na Gabriel Kilamlya Njombe

Mkazi wa Kibena Yuda James Anadaiwa Kutekwa na Kupigwa na Watu  Aliowataja Kuwa ni Wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Njombe na Kumsabashia Majeraha Katika Mkono Wake wa Kulia Wakimtuhumu  Kuhusika na Kuchana Mabango ya Mgombea Urais Dokta John Pombe  Magufuli.

Akizungumza na www.gabrielkilamlya.blogspot.com  Bwana Yuda Amesema Kuwa Tukio Hilo Limemkuta Septemba 20 Mwaka Huu Akiwa Katika Mtaa wa Kibena Ambako Alijikuta Anaitwa na  Mtu Aliyemfahamu Kwa Jina la Erasto Ngole na Kisha Kuingizwa Ndani ya Gari na Kupelekwa Katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Njombe Ambako Anadai Kupigwa na Kujeruhiwa Mkono Wake.

Amesema Kufuatia Tukio Hilo Alilazimika Kwenda Katika Kituo Cha Polisi Ambako Alipewa Fomu ya Matibabu PF3 na Kisha Kwenda Kutibiwa.

Mtandao Huu Umemtafuta Erasto Ngole Anayedaiwa Kufanya Tukio Hilo Ambaye Amekiri Kwenda Kumchukua Kibena na Kumpeleka Polisi na Sio CCM Kama Alivyosema Huku
Akikanusha Kuhusika Kumpiga na Kumjeruhi Mkono.

Amesema Sababu Iliyowafanya Kumfuata na Kumkamata ni Kutokana na  Kuhusika Kuchana Mabango ya Chama Cha Mapinduzi CCM Ya Mgombea Urais Dokta Magufuli.

Jitihada za Kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Ili Kuthibitisha  Tukio Hilo Zimegonga Mwamba Baada ya Kuelezwa Kuwa Kamanda Huyo Yupo Safarini.

Alatanga Nyagawa ni Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Njombe Ambaye Baada ya Kutafutwa Amelaani Vikali Kitendo Hicho na Kwamba Kinachotakiwa ni  Kufanya Siasa za Kistaarabu na Sio Kugombana Kwa Sababu za Kuchana  Mabango.


Hata Hivyo mtandao Huu Umefika Katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Ambapo Baada ya Kumkosa Katibu wa CCM Mkoa Bwana  Hosea Mpagike Jitihada za Kumtafuta Kwa Njia ya Simu Zikafanikiwa Kupata  Majibu Yakuwa Hana Taarifa Juu ya Tukio Hilo na Kushauri Atafutwe  Mtuhumiwa Mwenyewe.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles