Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

MIFUGO YAUWAWA KWA SUMU ISIMANI IRINGA

$
0
0

Mifugo  mbali mbali  iliyouwawa kwa  sumu katika mgogoro wa ardhi  kijiji cha Ismani  wilaya ya  Iringa
Ng'ombe  aliyeuwawa kwa  sumu
Wananchi  wa Kijiji  cha Isimani  wilaya ya  Iringa  wakitazama  mifugo  iliyokufa kwa  sumu
Mizoga ya  ng'ombe na  punda  ikiwa imezagaa ovyo  baada ya  kuuwawa  kwa  sumu
Mizoga  iliyokufa kwa  sumu
NG'OMBE  6 pamoja na  punda   watatu   waumeuwawa katika  mgogoro  wa  ardhi kwenye  kijiji   cha Isimani   kaya ya  Kihorogota   wilaya ya  Iringa  vijijini  baada ya kuwekewa   sumu ya  kuua  panywa katika  pumba   katika  shamba hilo  lenye mgogoro .

Wakizungumza na  mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz  baadhi ya   wafugaji  ambao  mifugo yao   imeuwawa  kwa  sumu  hiyo  walisema  kuwa   tukio  hilo  limetokea  juzi  majira ya  asubuhi  baada ya  mmoja kati ya   watu  waliopo katika mgogoro huo wa ardhi  kudaiwa  kuweka   sumu  hiyo.

Akizungumza kwa  niaba  ya  wenzake Geofrey Sanga  alisema    siku moja kati ya  tukio hilo mmoja kati watoto  wa mwenye shamba    hilo  alionekana  majira ya  jioni  katika  eneo hilo ambalo hata  hivyo  limekuwa  halilimwi  kwa muda  mrefu .

Hata   hivyo  siku ya pili  yake   kama kawaida  alipita  eneo hilo na  mifugo  yake   kuelekea  shamba na baada ya  kufika  eneo hilo  mifugo    hiyo  ilikula  pumba   hiyo ambayo  iliwekwa  sumu na  hivyo  kupelekea   kufa.

Alisema  kuwa  sumu hiyo  ilikuwa  imewekwa  katika pumba ambayo  ilimwagwa katika mae neo mbali mbali ya  shamba   hilo  .
    
Diwani wa kata ya  Kihorogota  COstantino  Kiwere  kulia  akimwonyesha  mmiliki wa mtandao wa matukio daima kaburi  lililotumika kuzika mizoga  hiyo
Hili ndilo eneo  mizoga  hiyo  ilipofukiwa
NG'OMBE  6 pamoja na  punda   watatu   waumeuwawa katika  mgogoro  wa  ardhi kwenye  kijiji   cha Isimani   kaya ya  Kihorogota   wilaya ya  Iringa  vijijini  baada ya kuwekewa   sumu ya  kuua  panywa katika  pumba   katika  shamba hilo  lenye mgogoro .

Wakizungumza na  mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz  baadhi ya   wafugaji  ambao  mifugo yao   imeuwawa  kwa  sumu  hiyo  walisema  kuwa   tukio  hilo  limetokea  juzi  majira ya  asubuhi  baada ya  mmoja kati ya   watu  waliopo katika mgogoro huo wa ardhi  kudaiwa  kuweka   sumu  hiyo.

Akizungumza kwa  niaba  ya  wenzake Geofrey Sanga  alisema    siku moja kati ya  tukio hilo mmoja kati watoto  wa mwenye shamba    hilo  alionekana  majira ya  jioni  katika  eneo hilo ambalo hata  hivyo  limekuwa  halilimwi  kwa muda  mrefu .

Hata   hivyo  siku ya pili  yake   kama kawaida  alipita  eneo hilo na  mifugo  yake   kuelekea  shamba na baada ya  kufika  eneo hilo  mifugo    hiyo  ilikula  pumba   hiyo ambayo  iliwekwa  sumu na  hivyo  kupelekea   kufa.

Alisema  kuwa  sumu hiyo  ilikuwa  imewekwa  katika pumba ambayo  ilimwagwa katika mae neo mbali mbali ya  shamba   hilo  .

Sanga alisema  kuwa  kwa  upande  wake  ni  pumba  watatu na ng'ombe  mmoja  ndio  waliokufa kwa  sumu hiyo  wakati  mwenzake  Chesco  Mdendemi  jumla ya ng'ombe  wake watatu   walikufa  huku  NIco Kahongole   sumu  hiyo  iliua ng'ombe wake  wawili 

Akithibitisha  kutokea  kwa  tukio hilo diwani  wa kata  ya  Kihorogota  alisema  kuwa  kuwa  hadi  sasa  tayari  kuna mtuhumiwa mmoja  amekamatwa  huku  msako  wa  kuwasaka  wengine  waliohusika na  uwekaji wa  sumu  hiyo  unaendelea  kufanywa na  wananchi kwa  kushirikiana na jeshi  la polisi .

Alisema  katika  eneo hilo la Isimani  kumekuwa na kero  kubwa ya panya na serikali  iliwapa  dawa ya  kuua panya  kutoka Morogoro  ila dawa  iliyotumika kuua mifugo   hiyo  si ile  ambayo  walipewa na  serikali .

Alisema  kuwa  eneo hilo  limekuwa na mgogoro  kwa  muda  mrefu  baada ya familia   kutaka  wananchi  wanaoishi eneo hilo  kuhama kwa madai kuwa  eneo la  hekari 300 katika  kijiji  hicho ni mali yao jambo ambalo  tayari  mahakama iliwapa  ushindi  wananchi  hao  kuendelea  kuwepo  eneo hilo.

Kwa hisani ya Francis Godwin

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles