![]() |
Transformer ya kiwanda cha karatasi mgololo yalipuka na kuwaka moto leo |
![]() |
Magari yakiwa eneo la Kiwanda hicho |
![]() |
Moto ukiendelea kuwaka katika eneo hilo la kiwanda cha karatasi mgogolo |
![]() |
Wananchi wakitazama moto huo |

![]() |
MOTO mkubwa umeteketeza kituo kikubwa cha umeme eneo la Kiwanda cha karatasi Mgololo wilayani Mufindi mkoani Iringa leo na kupelekea wilaya nzima ya Mufindi ,makambako na mkoa wa Mbeya kuwa gizani . Baadhi ya mashuhuda waliozungumza na mtandao wa www.matukiodaima.co.tz wamedai kuwa moto huo ambao ulianza kuwaka majira ya saa 4.5 asubuhi chanzo chake kinadaiwa ni hitirafu ya mitambo hiyo ya kusambaza umeme . Salum Omary ambae ni mmoja kati ya mashuhuda alisema kuwa eneo hilo ndilo lenye Transformer kubwa linalosambaza umeme katika kiwanda cha karatasi Mgololo ,wilaya nzima ya Mufindi , hadi mkoani Mbeya. Alisema kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea eneo hilo la Transformer hiyo kubwa wafanyakazi walilazimika kutimua mbio kutoka nje ya kiwanda hicho huku kiwanda kikizimwa ili kuepusha madhara zaidi kutokea . Hata hivyo alisema tatizo hilo la umeme si rahisi kurejea leo ama kesho kwani madhara ni makubwa zaidi na kuwa upo uwezekano wa wananchi wa wilaya ya Mufindi na mkoa wa Mbeya kuendelea kuwa gizani. " Toka eneo lilipokuwa Transforme hilo na kilipo kiwanda ni kama umbali wa Km moja hivi hivyo iwapo jitihada za haraka zisingefanyika huenda madhara yangejitokeza kwa kiwanda hicho cha karatasi mgololo" Meneja wa Tanesco mkoa wa Iringa hakuweza kupatikana kuendelea madhara zaidi yaliyojitokeza katika moto huo. Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu amethibitisha kutokea kwa moto huo na kuwa hakuna madhara kwa binadamu wala kiwanda hicho cha karatasi na kuwa moto huo umezimwa na gari la zimamoto la misitu ya Sao hill . Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa kwa sasa wilaya ya Mufindi hadi mkoa wa Mbeya upo gizani kutokana na tatizo hilo kubwa la umeme . Kwa hisani ya fg blog |