Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all 2276 articles
Browse latest View live

Article 0

$
0
0
Hii ni Mahakama ya Wilaya ya Njombe Ambayo kwa sasa Pia Inatumika kama Mahakama Kuu Mkoa wa Njombe.

Mahakama Kuu ya Mkoa wa Njombe Hii Leo Imemuhukumu Kifungo cha Miaka Nane Jela Benard Ngailo Mwenye Umri wa Miaka 35 Baada ya Kumkuta na Kosa la Kumuuwa Bila Kukusudia Kaka Yake Ronward Ngailo

Akitoa Hukumu Hiyo Jaji M.S. Shangari Amesema Mahakama Imetoa Adhabu Hiyo Baada ya Kusikiliza Hoja za Pande Zote Mbili , na Kwamba Mahakama Imeridhika na Ushahidi Uliotolewa na Upande wa Mashtaka na Kuongeza Kuwa Adhabu Hiyo Imetolewa Kwa Mshtakiwa Ili Iwe Fundisho Kwa Watu Wengine Wenye Tabia Kama Hiyo.

Ukitoa Utetezi Upande wa Mshtakiwa Uliomba Kupunguziwa Adhabu Hiyo Kutokana na  Mshtakiwa Ana Watoto Saba Wanaomtegemea na Amekaa Lumande Kwa Takribani Mwaka Mmoja.

Awali Akisoma Shtaka Hilo Mahakamani Hapo Wakili wa Serikali Francis Lojas Ameiambia Mahakama Kuwa Mshtakiwa Alitenda Kosa Hilo Aprili 20 Mwaka 2010 Majira ya Saa Tatu Usiku Katika Kijiji cha Igagala na Kuiomba Mahakama Itoe Adhabu Kali Kwa

Mshtakiwa.

Imedaiwa Mahakamani Hapo na Wakili wa Serikali Lojas Kuwa Siku ya Tukio Mshtakiwa Alimuuwa Ronward Ngailo Ambaye ni Kaka Yake Kwa Kumkata na Kitu Chenye Ncha Kali Sehemu za Kichwa na Mikono Pamoja na Kumtoboa Machao Kwa Bisibisi na Kisha Kutumbukiza Chaooni Kwa Kile Kilichodaiwa Kuwa ni Wivu wa Kimapenzi.

Wakati Huo Huo Mahakama Hiyo Imeshindwa Kutoa Hukumu ya Kesi ya Mauwaji Inayomkabili Sophia Mliulika Mkazi wa Mabengu Mkoa Njombe Kwa Kile Kinachodhaniwa Kuwa Mshtakiwa Ana Uwezekano wa Kuwa na Matatizo ya Akili.

Akitoa Hoja Hiyo Mahakamani Hapo Wakili wa Upande wa Utetezi Bwana Kingwe Ameiomba Mahakama Kabla ya Kutoa Hukumu Mshtakiwa Akafanyiwe Uchunguzi Kwani Alionekana Kuwa na Matatizo ya Akili, Hoja Ambayo Mahakama Hiyo Imelikubali.

Mshtakiwa Sophia Mliulika Anakabiliwa na Kesi ya Kumuuwa Mtoto Wake Kwa Makusudi.

Article 5

$
0
0

MGOGORO WA WANANCHI WA KIJIJI CHA IGUNDU CHUNYA MBEYA NA WAFUGAJI UMEMALIZIKA.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu Mweyekiti wa kijiji  cha IGUNDU EMMANUEL MBUGHI alipatanishwa na Mwenyekiti wa Wafugaji SAMWEL LAURENT ambao walipatanishwa na Afisa Tawala Wa Wilaya ambapo pande hizo ziliahidi kukomesha vitendo hivyo na kwamba wananchi wa IGUNDU waondoe hofu wao kama wafugaji hawatalipiza kisasi na waendelee na shughuli za uzalishaji mali

 Baada ya mwenzao kuuwawa na maiti kuibwa hospitali wafugaji wakiandamana kuelekea eneo la tukio kujua kulikoni
Kazi kweli kweli
Mweyekiti wa kijiji  cha IGUNDU EMMANUEL MBUGHI akijaribu kuwatuliza wafugaji hao kuwa watulie na wakae chini na kujadili huo mgogoro wao
Hakika wafugaji wakatulia na kusubiri viongozi ili waanza kujadili swala lao
Afisa Tawala Wilaya ya CHUNYA AMIMU MWANDELILE ambaye alilaani vikali kitendo kilichofanywa na vijana hao kwani kitendo hicho hakikubaliki na jamii kwani kinaondoa utu wa Mtanzania.

Mwenyekiti wa Wafugaji SAMWEL LAURENT  akielezea jinsi mgogoro huo ulivyoanza

Hakika hali ya amani imerejea tena sasa nifuraha tu


Hatimaye mgogoro baina ya wanakijiji cha IGUNDU Kata ya SANGAMBI wilaya ya CHUNYA  Mkoani MBEYA na jamii ya WAFUGAJI umemalizika baada ya serikali wilayani humo kuzikutanisha pande hizo na kuondoa tofauti zao.

Mgogoro huo uliodumu kwa wiki moja kufuatia baadhi ya vijana wa kijiji hicho kumuua mfugaji aliyefahamika kwa jina la SAID PETRO kwa kipigo kutokana na vijana hao kumtaka awape pesa naye kushindwa kutekeleza takwa lao ndipo walianza kumpiga.

Kabla ya kupatanishwa wafugaji hao walikutana faragha kutoa msimamo wao juu ya vitendo vilivyokithiri kutoka kwa wanakijiji cha IGUNDU wakidai hilo ni tukio la tano kutokea na serikali ya kijiji haijachukua hatua yoyote kukomesha vitendo hivyo.

Baada ya mjadala mrefu wafugaji walikubali kusogea meza ya mazungumzo yaliyoongozwa na Afisa Tawala Wilaya ya CHUNYA AMIMU MWANDELILE ambaye alilaani vikali kitendo kilichofanya na vijana hao kwani kitendo hicho hakikubaliki na jamii kwani kinaondoa utu wa Mtanzania.

AMIMU amesema vitendo vya uhalifu kijijini hapo vinachangiwa na unywaji wa pombe kupita kiasi na utumiaji wa madawa ya kulevya ambapo vijana wanatafuta njia ya mkato kutafuta pesa  ikiwemo kucheza kamali badala ya kufanya kazi.

Aidha amesema kuwa serikali haitafumbia macho vitendo hivyo atahakikisha wale wote waliohusika na vitendo hivyo wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kwani hakuna mtu yeyote aliye juu ya sheria hivyo anayevunja sheria hatavumiliwa kabisa.

Kwa upande wake AMIMU alichukua fursa hiyo kuwapongeza wafugaji hao kwa moyo wa uvumilivu kwa kutolipa kisasi pamoja na vitendo vya kikatili walivyofanyiwa wafugaji hao zaidi ya mara tano hata kupelekea wengine kujeruhiwa na wengine kuuawa.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu Mweyekiti wa kijiji  cha IGUNDU EMMANUEL MBUGHI alipatanishwa na Mwenyekiti wa Wafugaji SAMWEL LAURENT ambao walipatanishwa na Afisa Tawala Wa Wilaya ambapo pande hizo ziliahidi kukomesha vitendo hivyo na kwamba wananchi wa IGUNDU waondoe hofu wao kama wafugaji hawatalipiza kisasi na waendelee na shughuli za uzalishaji mali,

Picha na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu

Article 4

$
0
0
 Kushoto ni Aliyekuwa Mwandishi na Mwanachama wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Njombe[NPC] Amos Kaposo Enzi za Uhai Wake.
Katikati ni Marehemu Amos Kaposo Akiwa Nje ya Hospitali ya Kibena Kabla Hajahamishiwa Igogo Mbeya.

Taarifa za Awali zinaeleza Kuwa Marehemu Amos Kaposo Ambaye Alikuwa mwandishi wa Habari wa Gazeti la Changamoto na Mwanachama wa NPC Mkoa wa Njombe Amefariki dunia Usiku wa Jana Mkoani Mbeya Ambapo Mazishi yanatarajiwa Kufanyika Kesho Septemba 5 Mwaka Huu katika Kijiji cha Igogo nyumbani kwao Mbeya.

Marehumu Amos Kaposo Awali Alikuwa Akisumbuliwa na Mgongo Aliofanyiwa Upasuaji na kisha hali yake Kuendelea Kuwa Mbaya kwa Kipindi kirefu Sasa.

Mtandao huu Unatoa Pole kwa Ndugu,Jamaa wa Karibu na Msiba Huu Pamoja na Wanahabari wote Kwa Ujumla 

Taarifa zaidi Juu ya Taratibu Nyingine Mtaendelea Kupata.

Endelea Kufuatilia Mtandao Huu.

Mungu Aielaze Roho ya Marehemu Amos Kaposo Mahali Pepa Ameeeeeen.

Article 3

$
0
0

Na Gabriel Kilamlya Njombe
 
Mahakama Kuu ya Mkoa wa Njombe Leo Amemhukumu Kifungo Cha Nje Kwa Masharti George Ndendya[59] Mkazi wa Kivavi Makambako Baada ya Kukutwa na Hatia ya Kumuua Geofrey Mwalongo Ambaye Alikuwa Mkazi wa Kihesa Mjini Njombe Bila Kukusudia.

Akisoma Hati ya Mashtaka Mbele ya Jaji wa Mahakama Hiyo,Wakili wa Serikali Rodgers Francis Ameiambia Mahakama Kuwa Tukio Hilo Limetokea Januari 16 Mwaka 2011 Majira ya Saa Kumi na Nusu Jioni Katika Uwanja wa Mpira wa Amani Makambako Wakati wa Mechi Kati ya Timu ya Njombe Mji na Mbeya Road ya Makambako.

Wakili Francis Amesema Kuwa Marehemu na Mshtakiwa wakiwa Mashabiki wa Timu Hizo walikuwa wakishangilia Mpira uliokuwa Ukichezwa Siku ya Tukio Huku Mashabiki wa Timu ya Njombe Mji wakaanza Kumfuata Mshtakiwa Huyo na Kumtukana Kuwa ni Mchawi na Anafanya Timu yao Isishinde.

Kufuati Hali Hiyo Ilimfanya George Ndendya Kuondoka Eneo Hilo na Kuelekea Sehemu Nyingine Ndani ya Uwanja Huo Kitu Ambacho Bado Mashabiki wa Timu ya Njombe Mji Wakaendelea Kumfuata na Kumtolea Maneno ya

Kumdhihaki na Kumuita Mchawi.

Wakili Huyo wa Serikali Bwana Rodgers Francis Ameiambia Mahakama Hiyo Kuwa Majira ya Saa 11:30 Jioni  Marehemu Geofrey  Mwalongo Ambaye Alikuwa Mkazi wa Kihesa Mjini Njombe  Akiongozana na Mashabiki Zaidi ya 50 wa Timu ya Njombe Mji Akachukua Ubao Aina ya Banzi na Kisha Kumpiga Bwana George Ndendya Hali Iliyomlazimu Kuchomoa Kisu Alichokuwa nacho na Kumchoma Marehemu Tumboni Katika Kujihami.

Baada ya Tukio la Kumchoma Kisu Tumboni Marehemu,Askari Polisi Waliokuwa Eneo la Tukio Wakamuamuru Mshtakiwa Aweke Kisu Chini na Kisha Kumkamata na Kumfikisha Katika Kituo Cha Polisi Huku Marehemu Akiwahishwa Katika Kituo cha Afya Makambako Ambako Baadaye Wakamhamishia Katika Hospitali ya Mji wa Njombe Kibena.

Wakili Francis Ameongeza Kuwa Marehemu Pia Alikimbizwa Hadi Hospitali ya Rufaa Jijini Mbeya Kwa Matibabu Zaidi Ambako Mauti yalimkuta Mnamo Januari 17 Mwaka 2011 Baada ya Kuvuja Damu Nyingi Kwa Mujibu wa Dokta Yunis Mbaga Aliyeandika Ripoti ya Kifo Hicho.

Alfred Kingwe ni Wakili wa Upande wa Utetezi Ambaye Ameiomba Mahakama Impunguzie Adhabu Mshtakiwa Huyo Kutokana Mazingira ya Tukio Hilo Kwani Alikuwa Hana Namna ya Kujihami na Tukio Hilo Zaidi ya Kutumia Silaha ya Kisu Alichokuwa Nacho Kabla ya Kuvamiwa Zaidi na Mashabiki Walioongozana na Marehemu.

Sanjali na Hayo Lakini Pia Wakili Kingwe Amesema Kuwa Kwa Kuzingatia Umri wa Miaka 59 Alio nao Mshtakiwa,Kukaa Mahabusu Kwa Kipindi cha Miaka Miwili na Miezi Minne,Kuwa na Mke na Watoto Wanne Ambao Anawasomesha na Kwamba Hana Kumbukumbu nyingine ya Makosa Ya Jinai,Mahakama Hiyo Haina Budi Kumpunguzia Adhabu.

Kufuatia Utetezi Huo Ndipo Mahakama Kupitia Jaji Merry Shangali Ikapima Uzito wa Kosa na Muda Aliokaa Mahabusu Kwa Kutumia Kanuni ya 38 Ya Adhabu Kifungu cha Tatu Kilichofanyiwa Marekebisho Mwaka 2002 na Kuona Hakuna Sababu yakuendelea Kurejeshwa Jela na Kisha Ikatoa hukumu ya Kifungo cha Nje Kwa Masharti ya Kuto tenda Kosa Lolote la Jinai Katika Kipindi Cha Miezi 12.


KATIKA KESI NYINGINE

Mahakama Kuu ya Mkoa wa Njombe Leo Imemuachia Kwa Masharti ya Kuto Tenda Kosa la Jinai Katika Kipindi cha Miezi 12 Baton Ngulo [39] Mkazi wa Kijiji Cha Utewele Wilayani Njombe Baada ya Kukutwa na Hatia ya Mauaji ya Bila Kukusudia.

Wakili wa Serikali Bwana Rodgers Francis Ameiambia Mahakama Kuwa Baton Ngulo Alimuua Festo Ngulo Ambaye ni Ndugu Yake Mnamo Tarehe 3 Mwezi  Januari Mwaka 2009 Kwa Kumchoma na Kisu Sehemu za Paja la Mguu wa Kushoto Wakati wakiwa Katika Kilabu cha Pombe za Kienyeji Aina ya Ulanzi Kinachofahamika kwa Jina la Mhimbili Kilichopo Kijijini Humo.

Wakili Francis Amesema Kuwa Siku ya Tukio Mshtakiwa Alitoka Nje ya Kilabu Chake na Kwenda Uani Wakati Akirudi Akamkuta Marehemu Amechota Pombe yake Kwenye Lita Nne Akitokea Kwenye Kaunta ya Kilabu Chake Akiwa anaiba Baada ya Kumuuliza Akaanza Kutoa Maneno ya Kashfa Akisema Pombe yake ni Mbaya.

Aidha Ameongeza Kuwa Wakati Akiendelea Kumuuliza Marehemu Aliendelea Kuwa Mkali na Akampiga Mshtakiwa Kofi Ndipo Walipo anza Kupigana na Wakati Marehemu Alipokuta Anazidiwa Akakimbia Kwenda Kuchukua Kisu Kwenye Kilabu Chake na Kurejea nacho Akiwa na Lengo la Kumdhuru Mshtakiwa.

Ameongeza Kuwa Kufuatia Hatua Hiyo Mshtakiwa Akafanikiwa Kumnyang'anya Marehemu Kisu na Kisha Kumchoma Sehemu ya Paja la Mguu wa Kushoto na Kupoteza Maisha yake Papo hapo Baada ya Kuvuja Damu Nyingi Kwa Mujibu wa Dokta Maria Lupenza Aliyefika na Askari Polisi Eneo la Tukio Kuandika Ripoti ya Kifo hicho.

Wakili wa Upande wa Utetezi Bwana Alfred Kingwe Ameiomba Mahakama Kumpunguzia Adhabu Mshtakiwa Kutokana na Ugomvi Kuanzishwa na Marehemu Aliyekuwa Akiiba Pombe ya Mshtakiwa.

Wakili Kingwe Ameongeza Kwa Kusema,Kwa Kuwa Mshtakiwa Amekaa Gerezani Kwa Kipindi cha Miaka Mitatu na Miezi Mitatu Bila Kupewa Dhamana na Anafamilia ya Mke na Watoto Watatu Wanaosoma,Hajawahi Kuwa na Kumbukumbu ya Kosa Lolote la Jinai na Hakuisumbua Mahakama Hivyo Hana Budi Kupunguziwa Adhabu.

Baada ya Kusikiliza Upande wa Utetezi,Jaji wa Mahakama Hiyo  Bi.Merry Shangali Amesema Kwa Kutumia Kanuni ya 38 Ya Adhabu Kifungu cha Tatu Kilichofanyiwa Marekebisho Mwaka 2002 Mahakama Imeona Hakuna Haja ya Kumrejesha Gerezani Tena  na Hivyo Imemuachia Kwa Masharti ya Kuto tenda Kosa la Jinai Katika Kipindi cha Miezi 12.

...........................................................................................................................


Article 2

$
0
0

ASKOFU  WA KANISA LA EAGT MOSES KULOLA AMEZIKWA LEO JIJINI MWANZA.

 


 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiongoza wanachi kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Askofu wa EAGT Moses, Kulola 

Endelea Kufuatilia Picha za Taswira Mbalimbali ya Mazishi Hayo Yaliyofanyika Jijini Mwanza













Mchungaji Kadani Limbu ambaye ni Katibu wa Kanisa la EAGT Makao Makuu (Ujenzi) akisoma wasifu wa marehemu Askofu Kulola aliyezaliwa 1928 katika Kijiji cha Nyang’honge Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza na kujaliwa kupata elimu ya msingi (Middle School) na sekondari ya Bwiru Boys Mwanza kati ya mwaka 1946 hadi 1949 kuendelea na masomo na kupata Civil Technician.

Baada ya kumaliza na kupata utaalamu huo na kuajiliwa kuwa mtumishi wa serikali katika Halmashauri ya Mji wa Mwanza kama Mhandisi wa Mchoraji wa Ramani za majengo na Barabara wakati wa uhai wake aliamua kuacha kazi na kuanza utumishi wa mungu akifanya kazi kwa kutembea kila mahali akihubiri Injili kwa watu mbalimbali.

Wasifu huo ulimwelezea Askofu Kulola wakati wa utumishi wake wa kiroho kuwa  alikuwa akitembea kwa miguu kuanzia mwaka 1962 akihubiri neno la Mungu .Baada ya kuacha kazi za serikali mwaka 1951 alipatwa na matatizo na kuwahi kufungwa gerezani na kupigwa na bwana jela na kuumizwa vibaya muguu wake wa kushoto na kupelekea kupata kilema ambapo aliwekewa mguu wa bandia.

Marehemu Askofu Kulola ameacha mke na watoto 10 wajukuu 42 vitukuu 16 na amekuwa mutumishi wa kiroho tangu  akiwa na umri wa miaka 18 .
 
kwa Hisani ya Jumamtandablog.

breaking Newsssss

$
0
0
MWENDESHA PIKIPIKI AVUNJWA KIDOLE BAADA YA KUGONGANA NA GARI NJOMBE

 Mwendesha Pikipiki Aina ya T Better Yenye Namba za Usajili Hapo Juu Amepata Ajali ya Pikipiki Wakati Akijaribu Kumu Overtake Mwenye Gari Linaloonekana Hapo Hapo Upande wa Kushoto Kinyume na Sheria za Barabarani Hivi Punde.







 Upande wa Kushoto mwa Gari Hilo Ndipo Alipojigonga Bodaboda huyo na Kisha Kuvunjwa Kidole chake kidogo cha Mkono wa Kulia
Taarifa za Mashuhuda wa Tukio Hilo wamesema Kuwa Mwendesha Bodaboda Ndiye Mwenye Makosa kwani Alikuwa Akitaka Kuovertake Gari Upande usio wake kisha Kupata Ajali Hiyo Jirani na Ofisi za Tanesco Wilaya ya Njombe Mtaa wa Chaugingi Mjini Njombe.

Tukio Hilo Limetokea Jioni Hii Ikiwa ni Wiki ya Nenda Kwa Usalama Barabarani Litakalohitimishwa Wiki Mbili zijazo.

Article 0

$
0
0
AFISA UTUMISHI WA MANISPAA YA ILEMELA  KORTINI  KWA RUSHWA YA NGONO.


Afisa utumishi wa manispaa ya Ilemela ndugu Songoma leo amefikishwa mahakamani akikabiliwa na kesi ya rushwa ya ngono kwa mwalimu aliyekuwa akiomba kuhamishwa toka Ngudu kuja Mwanza.

Akisomewa shitaka lake mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya Mwanzo, ofisa wa TAKUKURU Bi. Debora amedai kuwa Songoma alitenda kosa hilo may tano mwaka jana ambapo maofisa wa TAKUKURU walifanikiwa kumtia mbaroni wakati
akijiandaa kupokea rushwa ya ngono ndani ya gesti moja jijini mwanza katika mtego ambao uliandaliwa na mwalimu huyo.

Hata hivyo, Afisa huyo amekana shitaka hilo na kesi yake imeahirishwa hadi septemba 13 mwaka huu.


kwa hisani ya VITUKO VYA MTAA Blog

Ripoti maalumu ya gazeti la MWANANCHI kuhusu vurugu zilizotokea jana bungeni

$
0
0

 

Jana, Bingwa wa Dunia wa uzani wa kati (super middle), unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBF), Francis Cheka alitembelea Bunge baada ya kutwaa taji hilo karibuni na jana hiyohiyo, Bunge hilo lilishuhudia ngumi kavukavu katika vurugu kubwa pengine kuliko zote zilizowahi kutokea katika ukumbi wake.

Katika masumbwi hayo yasiyo rasmi, Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ anadaiwa kumpiga kichwa Askari wa Bunge na kumchania sare na kung’oa kipaza sauti.


Mbilinyi jana alisema alikuwa anatafutwa na polisi huku akisema hilo limemshangaza akidai kwamba yeye ndiye aliyeshambuliwa na askari huyo.


Vurugu hizo zilitokea baada ya Naibu Spika, Job Ndugai kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.


Katika vurugu hizo Mbilinyi alibebwa juujuu na polisi hadi nje ya ukumbi huku akiwa hana viatu.


Pamoja na tafrani hiyo, Ndugai alisema wakati akihitimisha kikao cha Bunge kipindi cha asubuhi kuwa amewasamehe wabunge wote waliohusika na kosa hilo la utovu wa nidhamu na kuwaruhusu kurejea kipindi cha jioni kuendelea na Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. 

Hata hivyo, wabunge wote CUF, NCCR-Mageuzi na Chadema ambao baada ya tukio hilo walitoka nje ya ukumbi, hawakurejea na baadaye walitoa msimamo wa pamoja wakisema hawatashiriki katika mjadala huo.


Msimamo huo ulitolewa na Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Mbunge wa CUF, Habib Mnyaa.


Mbowe alisema wameamua kususia majadiliano hayo kuonyesha msimamo wao wa kupinga kupitisha mambo yasiyo na masilahi kwa nchi.
 
“Hatuko tayari kushiriki katika uchakachuaji wa Katiba... Matumizi ya nguvu ya polisi kamwe hayatatupatia Katiba nzuri,” alisema. Alisema kambi rasmi ya upinzani inalaani vikali kitendo cha Ndugai kuruhusu Bunge kunajisiwa kwa kuruhusu polisi kuingia ndani kinyume na kanuni.


Mnyaa alisema kitendo cha wadau wa Zanzibar kutoshirikishwa katika kutoa maoni yao katika muswada huo wa marekebisho ni dharau kubwa.


Mbatia alisema Tanzania haiwezi kuingia Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kutumia Katiba ya sasa kwa sababu tayari kuna mgongano wa kikatiba kati ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alimtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kutoa ushahidi kama Rais aliteua wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kulingana na mapendekezo ya taasisi zao.

Kuanza kwa tafrani
Sakata hilo lilianza saa 6:45 mchana muda mfupi baada ya kukamilika kwa kura kuamua kama Bunge liahirishwe au la kutokana na hoja iliyotolewa na Mbunge wa Mkoani (CUF), Ali Hamisi Seif (CUF). Waliotaka liahirishwe walipata kura 59 na waliokataa 159.

Baada ya Ndugai kutangaza matokeo hayo na kutaka shughuli za Bunge ziendelee, Mbowe aliposimama na kusema ana hoja Naibu Spika alimwamuru akae chini.

Baada ya Mbowe kusisitiza ana hoja na kumwomba Spika amsikilize ndipo Ndugai alipomwamuru atoke nje na alipokaidi alisema:” Naomba askari wote waliopo katika mazingira haya (ya Bunge) waingie ndani ya ukumbi wa Bunge”.

Baada ya kitambo kifupi, Mbowe akiwa bado amesimama alitoa maagizo atolewe nje: “Kiongozi wa upinzani atolewe nje.”

Polisi waliingia ndani ya Ukumbi wa Bunge lakini Wabunge wa Kambi ya Upinzani kwa umoja wao, walimzinga Mbowe asifikiwe na askari hao.

Baada ya kuona polisi wanaelekea kushindwa, Ndugai alitoa maagizo mengine: “Askari hamjaletwa humu ndani kufanya majadiliano mnatakiwa kuhakikisha kiongozi wa upinzani anatolewa nje”.

Alisema yeye ndiye anayeendesha kikao hicho hivyo lazima Mbowe atolewe nje.

Hapo ndipo wabunge hao wa upinzani walipoanza kuimba: “Hatutaki kuburuzwa hatutaki kuburuzwa… hatutaki kuonewa,” huku wakiendelea kumzinga Mbowe.

“Askari wote mliopo humu ndani naomba mnisikilize… Sasa naagiza kwa mara ya mwisho... nasema kiongozi wa upinzani atolewe nje.”

Ngumi zarushwa
Baada ya kauli hiyo ya Ndugai, ndipo polisi walipotumia nguvu hasa kwa Mbilinyi na Mbunge wa Maswa Mashariki (Chadema), Silvester Kasulumbai.

Katika patashika hiyo, inadaiwa kwamba Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali alipigwa ngumi ambayo ilimfanya apepesuke hadi sakafuni.

Kilichomponza Mbilinyi ni hatua yake ya kusogelea Siwa. Polisi waliokuwa karibu, walimbeba juujuu hadi nje ya ukumbi.

Wakati akitolewa nje ya ukumbi, alijaribu kujizuia kwa kushika kipaza sauti kinachotumiwa na upande wa upinzani hadi kikang’oka.

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Mozza Abeid, alivuliwa hijabu katika vurumai hizo wakati polisi walipokuwa wakitumia nguvu ili kumfikia Mbowe.

Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, Mbowe aliamua kutoka nje huku akisindikizwa na polisi pamoja na wabunge wa vyama hivyo na alipofika nje ya ukumbi alipokewa na polisi wa kawaida waliomweka chini ya ulinzi kabla ya kumwachia baada ya ombi la Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini.

Kutokana na hali ya mambo kuwa tete, askari wa Bunge waliwaondoa wageni waliokuwa wamekaa katika kumbi za wageni wakiwamo wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari huku baadhi ya wabunge wa CCM waliokuwa na simu za kisasa za mkononi na kompyuta mpakato (Ipad) wakichukua picha za tukio zima.

Inadaiwa kwamba baada ya kutoka nje ya ukumbi, Mbilinyi alimtwanga ngumi mmoja wa askari waliomtoa kwa nguvu kabla ya kuamuliwa na wabunge na polisi.
Wakati wote huo, wafanyakazi wa Bunge na wageni walionekana wakiwa wamejikusanya katika makundi wakitafakari na kushangaa yaliyokuwa yakitokea.

Balaa lilivyoanza
Akitumia Kanuni ya 69(1), Mbunge wa Mkoani (CUF), Ali Hamisi Seif, alitaka kuahirishwa kwa mjadala wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013 kutokana na ukweli kuwa Kamati ya Sheria, Katiba na Utawala ya Bunge ilipaswa kukusanya maoni ya wadau mbalimbali nchini ikiwamo upande wa Zanzibar jambo ambalo halikufanyika wakati wa maandalizi ya muswada huo.

“Ilipaswa sheria hii inapotaka kufanyiwa marekebisho iende tena kulekule Zanzibar lakini jambo la kusikitisha kamati inayohusika na masuala ya Katiba haikwenda. Mimi ni mjumbe wa kamati na tuliitwa Dar lakini ratiba waliyotupa haikuonyesha kama tungekwenda Zanzibar,” alisema. 

Mkosamali naye aliomba mwongozo kwa Spika, akisema kwa kuzingatia matakwa ya kiapo cha Spika au Naibu alipaswa kuendesha Bunge kwa haki bila upendeleo.

“Kanuni inasema Spika ama Naibu Spika ama Mwenyekiti ataendesha shughuli za Bunge kwa haki, uadilifu, bila chuki wala upendeleo wowote kwa kuongozwa na Katiba ya nchi,” alisema na kuongeza: “Kwa kuwa sisi tumekuweka hapo ili uendeshe Bunge kwa uadilifu, usiburuzwe na chama chako na uzingatie miongozo yote kwa wakati. Kwa nini usitumie mamlaka yako kuondoa muswada huu”?

Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenister Mhagama aliomba mwongozo kwamba kwa kuwa bado kuna malalamiko basi waipe Serikali nafasi ya kuthibitisha kwamba majadiliano ya kamati yalikamilika.

Lissu katika kuomba mwongozo wake, alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala, Pindi Chana alilidanganya Bunge alipowasilisha maoni ya kamati kwamba wadau wa muswada huo walishirikishwa jambo ambalo alisema si kweli.

Lissu alisema hakuna Mzanzibari aliyefika mbele ya kamati hiyo kutoa maoni kuhusu muswada wowote.

Hata hivyo, Chana alijibu akisema wadau wa Zanzibar walitoa maoni yao na kukabidhi nyaraka mbalimbali kwa Spika kuthibitisha kauli yake hiyo. Alivitaja vyama vya Jahazi Asilia na ADC kuwa vilihojiwa.

Kwa upande wake, Lukuvi alimshambulia Lissu kwa kauli yake ya juzi kwamba uteuzi wa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete ulikuwa na walakini. “Lissu alisema jana (juzi) kwamba wapo wadau ambao walisema ijapokuwa waliandikiwa barua ya kuwasilisha majina matatu kila moja ili Rais ateue mmoja lakini hakuna mjumbe aliyeteuliwa”.

Alitaja majina ya walioteuliwa kuwa ni Maria Kashonda (Tec), Jesca Mkuchu (CCT), Humphrey Polepole (Civil Society) na Profesa Palamagamba Kabudi (Kundi la Wasomi).

Lukuvi aliwataja wengine waliopendekezwa na taasisi zao na Rais kuwateua kuwa ni Mwamtumu Malale (Bakwata) na Dk Sengondo Mvungi (NCCR) na Profesa Mwesiga Baregu wa Chadema.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Fredrick Werema alisema katika mchakato wa muswada huo, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) iliwasilisha maoni yake mbele ya kamati.

Alisema Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi aliwasilisha kwa kamati mapendekezo ya SMZ, Mei mwaka huu na mapendekezo hayo ikiwamo uteuzi wa wajumbe 166 yalizingatiwa.


Waacha muswada, wapiga vijembe
Baada ya kurejea katika kikao cha Bunge cha jioni jana, wabunge wa CCM waliopewa fursa ya kuchangia mjadala wa muswada huo walitumia muda mwingi kuwajadili wabunge wa kambi ya upinzani.

Article 7

$
0
0

 Na Gabriel Kilamlya Njombe

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Imejihakikishia Kupata Shilingi Milioni 344.4 Kwa Mwaka Kutoka kwenye Vyanzo vya Mapato Mbalimbali Kutoka Kwenye Kata Tatu zilizobinafsishwa Vyanzo Vyake.

Kata Hizo ni Zile za Matembwe,Kidegembye na Ikuna Ambazo Kuanzia Septemba Mosi Mwaka Huu Vyanzo vyake vya Mapato Vyote Vimebinafsishwa Ili Kuongeza Kiwango cha Ukusanyaji Mapato Pamoja na Kuwapunguzia Majukumu ya Kusimamia Shughuli za Maendeleo Maafisa Watendaji  wa Vijiji na Kata.

Akizungumza na www.gabrielkilamlya.blogspot.com Juu ya Suala Hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bwana Valence Kabelege Amesema Kuwa Hatua Hiyo Imekuja baada ya Kubaini Kupungua Kwa Mapato Kutokana na Usimamizi Mdogo na Baadhi ya Watendaji Kuto Kuwa Waaminifu Katika Zoezi la
Ukusanyaji Mapato Hayo.

Aidha Amesema Kuwa Majukumu Mengi ya Watendaji Yalikuwa Yakipelekea Baadhi ya Mapato Kutoroshwa na Hivyo Halmashauri Kukosa Mapato yake Ikizingatiwa Halmashauri Hiyo Kuwa na Kata 11 Pekee kati ya 28 Zilizokuwepo Hapo Awali.

Pamoja na Mambo Mengine Bwana Kabelege Amesema Kutokana na Mapato yatakayo patikana Kutoka Kwenye  Kata Hizo Tatu  Basi yatatoa Majibu ya Kubinafsisha na Kata Nyingine Zote au Kuendelea na Utaratibu wa Zamani Kuanzia Mwaka Mwingine wa Fedha.


Kwa Upande wake Afisa Uhusiano wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bwana Lukelo Mshaura Amesema Endapo Suala Hilo na Makubaliano ya Mkataba na Mzubuni Huyo Yatakwenda Sawa Basi Itakuwa ni Karibu Mara Mbili ya Mapato yaliyokuwa Yakikusanywa na Maafisa Watendaji waliopo.

Article 6

$
0
0

KIKWETE NA KAGAME WAKUBALIANA.

9676683911_4bb4b2c005_z_6f8c2.jpg

Rais Jakaya Kiwete wa Tanzania (kulia) na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakipeana mkono wakati walipokutana kwenye ICGLR Summit mjini Kampala Uganda leo.(Jana)
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 5, 2013, amekutana kwa faragha na Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame katika mazungumzo yaliyokwenda vizuri na kuwaridhisha viongozi hao wawili wa nchi jirani.

Viongozi hao wamekutana kwa zaidi kidogo ya saa moja katika mkutano uliofanyika kwenye Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, nje kidogo ya mji wa Kampala, Uganda.
Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete na Rais Kagame wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kujenga 
uhusiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili.

Viongozi hao wawili wako nchini Uganda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Kimataifa wa Maziwa Makuu – “International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR)” unaofanyika leo Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort.

Viongozi wengine ambao wanahudhuria Mkutano huo ni pamoja na Rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye ni Mwenyekiti wa ICGLR na mwenyeji wa Mkutano huo, Rais Silva Kiir wa Sudan Kusini, Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU).

Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili Kampala asubuhi ya leo Septemba 5 akitokea mjini Dodoma ambako aliwasili jana jioni kwa ajili ya hafla ya kuwaapisha Makatibu Wakuu watatu na Naibu Makatibu Wakuuu wawili iliyofanyika Ikulu Ndogo, Dodoma.

Rais Kikwete aliwasili Dodoma akitokea Mwanza ambako alihudhuria mazishi ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu Mkuu Dkt. Moses Samwel Kulola yaliyofanyika kwenye Kanisa la Bugando Calvary Temple, mjini Mwanza.

Imetolewa na;Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,Ikulu,DAR ES SALAAM.

Article 5

$
0
0

GARI LAPINDUKA UWEMBA NJOMBE .

 

 Wananchi  wa  Uwemba  wilaya ya Njombe wakishuhudia  ajali ya  gari 

 Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa  Deo Filikunjombe  kulia  akishuhudia  ajali  ya gali lenye  namba T570BNP ambalo  lilipinduka  na  dereva  wake  mwenye koti  jekundi  akiwa amechomoka katika gari  hilo ambalo lilikuwa na abiria  mmoja ambae  pia amepona
 Abiria  wa  gari  hilo akiruka  katika  gari  hilo baada ya  ajali  kutokea

 Abiria  aliyekuwemo katika gari hilo akijiokoa  kwa  kuruka katika gari  mara  baada ya  kupinduka eneo la Uwemba  barabara  kuu ya Njombe - Ludewa
 
KWA Hisani ya Francis godwin

Article 4

$
0
0

DEREVA BODA BODA AUAWA  KINYAMA IRINGA


Edger Lalika akiwa  wodini kabla ya  kufariki dunia.................................................................................
 _______________________________________________________
 Francis Godwin na  kayanda manyanya,Iringa 

Zikiwa  zimepita  siku  chache  toka  mmoja kati ya madereva boda boda mjini Iringa kutekwa kisha  kujeruhiwa vibaya kablaya kuporwa  pikipiki  yake ,unyama huo dhidi ya madereva  boda boda  umeendelea kutikisa mji wa Iringa baada Kijana mmoja mkazi wa kihodombi kutekwa kisha kuuwawa kinyama.
Tukio hilo la kinyama  limetokea  usiku  wa  leo baada ya kijana  huyo aliyetambulika kwa  jina la Edger Lalika kukutwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani .
Mashuhuda  wa  tukio hilo  wameueleza mtandao  huu wa matukio daima .com kuwa tukio la kuuwawa  kwa  dereva  boda  boda  huyo liletokea eneo la 
Tosamaganga wilaya ya Iringa mkoani Iringa.
Hata  hivyo kijana  huyo anayekadiliwa  kuwa na umri wa miaka 20,ameuwa akiwa anafanya shughuli zake za bodaboda baada  ya  kukodiwa na mteja  wake huyo ambae aliamua  kuitoa roho yake kabla ya kumpokonya boda boda.
Kutokana na tukio  hilo  baadhi ya madereva bodaboda wamelaani vikali kitendo hicho na kuwataka madereva bodaboda wengine kuungana na kushirikiana na jeshi la polisi kufichua vitendo hivyo  vya utekaji na mauwaji  dhidi ya madereva  boda boda.
 Mazishi ya kijana huyo yanafanyika leo katika makaburi ya mlolo Iringa mjini

Jeshi la  polisi mkoa  wa Iringa  limethibitisha  kutokea kwa mauwaji  hayo.

Article 3

$
0
0

KATIBU MKUU MPYA SIXTUS MAPUNDA AKABIDHIWA OFISI YA UVCCM

KATIBU Mkuu mstaafu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigela (kushoto) akimkabidhi Katibu Mkuu mpya wa UVCCM, Sixtus Mapunda, faili wakati wa makabidhiano ya Ofisi, waliyofanya, Makao Makuu ya UVCCM, mjini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni, Naibu Katibu Mkuu UVCCM (Bara), Mfaume Ally Kizigo na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Utekelezaji UVCCM Taifa, Seki Kasuga.  (Picha na Bashir Nkoromo).

WANAHABRI NA MAOFISA WA BUNGE WAPATA AJALI

$
0
0
IMG-20130905-WA0010IMG-20130905-WA0006 (1)
IMG-20130905-WA0005

IMG-20130905-WA0008Gari lilivyopinduka
  Afisa Habari wabunge Owen Mwandumbya akiwa amepumzishwa ili apate hewa kidogo baada ya ajari <
IMG-20130905-WA0006IMG-20130905-WA0005 (1)IMG-20130905-WA0003
Matukio ya picha baada waandishi na maafisa wabunge walivyonusurika katika ajari iliyotokea karatu jana.
Maafisa wa Bunge na waandishi walikuwa katika msafara wa Wabunge toka nchi za SADC waliokua wanaelekea ngorongoro( na Fullshangwe Blog)

Article 1

$
0
0



Gari la Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Kilifanikiwa Kufika Japo kwa Kuchelewa na Kisha Kuzima Moto Huo kwa Kushirikiana na Wananchi.

Na Gabriel Kilamlya NJOMBE,

Wananchi wa Mtaa wa Mjimwema na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mjini Njombe Wamefanikiwa Kuzima Moto Uliokuwa Unawaka na Kuuguza Zaidi ya Hekari 20 za Mashamaba ya Miti Yaliyokaribu na Mto Eneo la Mjimwema.

Wakieleza Chanzo cha Moto Huo Baadhi ya Mashuhuda Wamesema Umetokana na Mtoto Tony Mligo  Mwanafunzi wa Darasa la Pili Katika Shule ya Msingi Mjimwema Mjini Wakati Akiwa  Kwenye Shughuli za Kuandaa Shamba Ambaye Alikimbia Baada ya Kutokea Moto.

Kwa Mujibu wa Dina Mligo Ambaye ni Mdogo wa Tony Amesema Kaka Yake Tony Mligo Alikuwa Akizuiliwa Kuwasha Moto  Lakini Hakuta Kusikia Hali Iliyopelekea Moto Huo

Kuzuka na Kuunguza Miti ya Mbalimbali Ambayo Thamani Yake Haijafahamika.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Mjimwema Andreas Mligo Amesema Licha ya Serikali ya Mtaa Kutoa Elimu na Kuzuia Shughuli za Uandaaji wa Mashamba Kwa Kuchoma Moto Bado Baadhi ya Wananch Wanakaidi Agizo Hilo.

Miongoni Mwa Wananchi Walioathirika na Moto Huo ni Bwana Fortunatus Mbilo Ambaye Ameuliwa Shamba la Miti la Hekari Sita.

Hivi Karibuni Serikali Wilayani Njombe Amepiga Marufuku Kuanda Mashamba Kwa Kuchoma Moto Pamoja na Kuendesha Shughuli za Kilimo Karibu na Vyanzo Vya Maji Lakini Bado Baadhi ya Wananchi Wanoaoneka  Kukaidi Agizo Hilo.

............................................................................................

JK AZINDUA MRADI WA KUFUA UMEME MWANZA.

$
0
0


Maelfu ya Wakazi wa Mwanza Wakimsikiliza Rais Kikwete Jana.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia maelfu ya wakazi wa Mwanza na miji ya jirani katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza leo jioni.Rais Kikwete yupo Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo Picha na Freddy Maro



 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa na kubonyeza kitufe kuashiria kuzindua mradi wa kufua umeme wa megawati 60 huko Nyakato,Mwanza leo asubuhi.Kushoto ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo.Uzinduzi wa mitambo hiyo ni
sehemu ya ufumbuzi wa tatizo la umeme uliokuwa unaikabili kanda ya ziwa.


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mitambo ya kufua umeme wa megawati 60 muda mfupi baada ya kuzindua mitambo hiyo huko Nyakato Mwanza leo. 

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (kulia akiwa na mavazi maalumu) akikagua jengo la upasuaji katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana,Mkoani mwanza leo mchana.
 
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumapili, Septemba 8, 2013, amezindua mtambo wa kufua umeme kiasi cha megawati
60 katika eneo la Nyakato mjini Mwanza, umeme ambao utachangia kwa kiwango
kikubwa kupunguza shida ya umeme katika Mkoa wa Mwanza na mikoa ya jirani.


Aidha,
Rais Kikwete ameiangiza Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme
Tanzania (TANESCO) kuanza mara moja maandalizi ya kupeleka umeme kwenye
machimbo ya madini ya nikeli yaliyoko Kabanga, Ngara, Mkoa wa Kagera.


Vile
vile, Rais Kikwete amesema kuwa Serikali yake itaharakisha mipango ya kujenga
reli hadi kwenye eneo hilo kama maandalizi ya kuanza kuchimbwa kwa madini hayo
ambayo ni mazito na kuyasafirisha kwa barabara kwenda bandarini Dar Es Salaam
kutaharibu kwa haraka barabara zinazojengwa kwa gharama kubwa nchini.


Akizungumza
kabla ya kuzindua mtambo huo, Rais Kikwete  ameitaka Wizara ya Nishati na Madini
kuharakisha mipango ya kuunganisha eneo la Kabanga, Ngara, Mkoani Kagera kwenye
Gridi ya Taifa ili uzalishaji wa madini ya nikeli usije kukwamishwa na ukosefu
wa umeme. Amesema kuwa mgodi huo utahitaji umeme mwingi kiasi cha megawati 40.


Rais
amesema kuwa Serikali yake itahakikisha inafikisha reli kwenye eneo la Kabanga
mapema ili kuhakikisha kuwa nikeli inayozalishwa inasafirishwa kwa reli badala
ya barabara. Amesema kuwa madini hayo ni mazito mno na kuyasafirishwa kwa
barabara kutaharibu kabisa na katika muda mfupi barabara ambazo zinajengwa
nchini kwa gharama kubwa.


Mtambo
wa Umeme wa Nyakato wenye uwezo wa kuzalisha megawati 60 ulianza kujengwa mwaka
jana, 2012, baada ya Serikali ya Tanzania kutiliana mkataba wa ujenzi na
Kampuni ya Semco and Rolls Royce ya Norway mwaka 2011 wakati maandalizi ya
ujenzi huo yalipoanza.


Gharama
za ujenzi wa mtambo huo ambazo ni sh bilioni 130 (Euro milioni 48.7 na dola za
Marekani 15.9) zimelipwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Tanzania.


Akizungumza
na wananchi kwenye sherehe ya uzinduzi huo, Rais Kikwete amesema kuwa umeme
siyo anasa bali ni moja ya vigezo vya msingi na muhimu kabisa vya maendeleo.


“Vipo
vigezo vingi vya maendeleo ya nchi na binadamu, lakini moja ya vigezo hiyo ni
umeme. Na ukiangalia matumizi ya umeme kwa kila nchi yanaonyesha kiwango cha
maendeleo cha nchi hiyo. Katika Marekani, kwa mfano, kila mwananchi anatumia
kiasi cha kilowati 12,000 kwa wastani. Sisi katika Tanzania ni kilowati 89 tu
na wastani wa Bara la Afrika ni kilowati 150,”
amesema Rais Kikwete na kuongeza:


“Nc
hi yetu ya Tanzania ina umeme kiasi cha megwati 1,450 tu wakati katika Afrika
Kusini ni megawati 45,000 na unaweza kuona tofauti ya maendeleo. Hivyo, ni
muhimu sana kwetu kuongeza kiwango cha kuzalisha umeme katika nchi yetu.”


Katika
siku ya tatu ya ziara yake kukagua miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mwanza,
Rais Kiwete pia amefungua Kituo cha Polisi cha Nyakato ambacho kimegharimu sh
milioni 450, Serikali ikiwa imechangia kiasi cha asilimia 20 cha gharama hizo.


Kituo
hicho cha kisasa kilianza kujengwa mwaka 2003 lakini ujenzi wake ukawa
unakwamakwama kutokana na ukosefu wa bajeti hadi uongozi wa polisi wa Mkoa wa
Mwanza ulipoamua  kukijenga kituo hicho
kwa njia ya kuishirikisha jamii na ikaundwa Kamati ya Ujenzi chini ya uenyekiti
wa Bwana Alfred Wambiura.

 
Akizungumza kwenye sherehe ya ufunguzi wa kituo hicho, Rais Kikwete ameahidi kuwa atajenga
nyuma moja kwa ajili ya mkazi ya polisi. Kituo hicho kina jumla ya askari
polisi 65.


KWA Hisani ya Michuzi blog

Article 3

$
0
0
WEZI WA NGURUWE WAKAMATWA NJOMBE. 
Kamanda wa Polisi Mkoani Njombe ACP Fulgency Ngonyani
 
Mkazi Mmoja wa Kijiji cha Mbugani Kata ya Mavanga Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe Teofrida Mgimba[16] Amefariki Dunia baada ya Kujinyonga na Kwa Kutumia kamba ya Manila Katika Kile kinachodaiwa ni wivu wa Mapenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe ACP Fulgency Ngonyani Amesema Tukio hilo Limetokea Septemba Nane Mwaka Huu Majira ya Saa Saba Mchana Katika Kijiji Hicho.

Kamanda Ngonyani Amesema Kuwa Katika Tukio Jingine septemba 7 Paulo Mhofi[22]Mkazi wa Kijiji cha Ikondo alifariki Dunia Baada ya Kutumbukia Kwenye Mto Kwepa kwa Muda wa Siku Nne na Kupelekea Mwili huo Kuanza Kuharibika.

Aidha Kamanda Ngonyani Amesema chanzo cha Tukio Hilo Bado hakijafahamika na Jeshi la Polisi Linaendelea na Uchunguzi ili kujua Kiini cha Tukio Hilo.

Wakati Huo huo watu Wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Njombe kwa Tuhuma za Kuiba Nguruwe wawili Wenye Thamani ya Shilingi Laki Saba Mali ya Kilian Mbena Mwenye Umri wa Miaka 30 na Mkazi wa Kijiji cha Mlowa Katika Halmashauri ya Mji wa Makambako Wilayani Njombe.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoani Njombe Inasema Kuwa Watu hao walikamatwa Septemba Tano Mwaka Huu Majira ya Saba Mchana Ambapo Sijaly Nyalusi[26] na Jely Nyalusi[26]wote wakazi wa Maguvani Makambako walikamatwa na Jeshi la Polisi Katika Maeneo ya Ubena Mjini Makambako Baada ya Kuiba Nguruwe Waliokuwa Kwenye zizi.

Amesema Kukamatwa kwa Wezi huo Kumetokana na Uchunguzi Uliofanyika na Ushirikiano kutoka kwa Wananchi.

Aidha Mnamo Septemba 8 Majira ya Tatu Asubuhi Katika Kijiji cha Wanging'ombe Katika Barabara kuu ya Makambako Mbeya Gari yenye Namba T 450 AEJ Toyota Chaser Saloon Mali ya Antony J Iliyokuwa ikiendeshwa na Dereva Ambaye hakufahamika Mara moja Iligonga gari lenye namba T 402 CFR Toyata Noah Mali ya Elice Joseph Iliyokuwa Ikiendeshwa na Peter Clavely Mwenye Umri wa Miaka 33 Ambaye ni Askari  wa JWTZ Kikosi cha 661 KJ.

Kamanda Polisi Ameeleza Kuwa Kutokana na ajali hiyo Ilipelekea kifo cha Abiria Mmoja na Kusababisha majeruhi kwa Vasco Mlowe wa Mbeya na Joseph Mtuka wa Sumbawanga na kwamba Ajali hiyo ilisababishwa na uzembe wa dereva wa gari aina ya  Chaser ambaye alishindwa kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Ameongeza kuwa baada ya tukio hilo dereva wa gari hilo alikimbilia kusiko julikana na jeshi la Polisi Linaendelea na Uchunguzi wa Tukio hilo.
 

Article 2

$
0
0
RTO NJOMBE ATOA ELIMU KWA MADEREVA WA BODABODA

 Kamanda wa Kikosi cha Nenda kwa Usalama Barabarani Mkoani Njombe Maro Chacha Akizungumza na Madereva wa Bodaboda Mchana Huu Katika uwanja wa NHC Mjini Njombe.
Bodaboda wapewa Elimu ya Nenda Kwa Usalama barabarani Mkoani Njombe na RTO.

Elimu Hiyo Inatolewa Kufuatia Kuimarisha Wiki wa Nenda Kwa Usalama Barabarani itakayohitimishwa Septemba 23 Mwaka Huu.

Ajali za Barabarani zinazosababishwa na Bodaboda zimeonekana kushamiri Mkoani Njombe Hali inayohatarisha Maisha ya Abiria na Wananchi Kiujumla.

Article 1

$
0
0
NI VIGEZO GANI HUTUMIKA KATIKA KUSHINDA TUZO YA USAFI WA MAZINGIRA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE?

Hili ni dampo Lililopo Nyuma ya Stendi Kuu ya Mabasi Mjini Sehemu Ambayo Biashara za Nguo na Vyakula zinafanyika.

Dampo Hili Mara kwa Mara Linaonekana Kujaa na Kuhatarisha Afya za Wakazi wa Maeneo hayo Kutokana na kushamiri kwa Uchafu kitu kinachopelekea Dampo hilo Kujaa hadi Taka Kumwagikia Pembeni  kama Linavyoonekana Hapo.

Leo Septemba 10 2013 mtandao huu Umetembelea Dampo Hili na Kushuhudia Hali Hii,na Njia Karibu Inaziba.

Mbali na Dampo Hili Kuwa Jirani na Mama Lishe wanaopika Vyakula na Wafanyabiashara wa Nguo za Mitumba kushinda Humo Ndani Lakini Pia Taka Hizo Zipo jirani kabisa na Kituo cha Afya Cha Njombe Mjini Ambako Hata Afisa Afya Yupo Jirani na Dampo Hili.

Halmashauri ya Mji wa Njombe ndio yenye Mamlaka ya kuhakikisha Inafanya Usafi Katika Eneo hili kwa Kuwa Huchukua Ushuru kwa Wafanyabiashara hao.

Wakala anayefanya kazi Hii Awali Alikuwa Akilalamikia Kuto lipwa Fedha yake sasa haijulikani kama Kazila au Kasusia kwa Muda.

Lakini Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Mji wa Njombe Imekuwa Ikishinda Mashindano ya Usafi wa Mazingira Karibu Kila Mwaka,Swali langu'.je ni
vigezo gani Hutumika?

Au Halmashauri hii hushinda kwa kuangalia usoni mwa Barabara tu ambamo usafi huonekana ukifanywa?

Salamu za Mjomba zilitembea sana lakini mwisho wa Siku zika ishia hapa"SAFARI IMENISHINDA SASA NARUDI KWETU"

Haina maana Kuwa Mjomba Kazi Ili Mshinda lakini aliona Kuwa Anaweza Kutumia Nguvu kubwa hadi kujisababishia Matatizo kwa kupiga Kelele Bila Mafanikio.

Hizi ni salamu za mtandao huu wa www.gabrielkilamlya.blogspot.com.

Hata wewe pia waweza Kutoa Ushauri Pia kwa Halmashauri yetu,Labda haina Bajeti ya Usafi katika eneo hili au, Inampango wa Kuwasusia wakazi wa Maeneo haya.

Lakini hata Wafanyabiashara wa Nguo katika eneo Hili waliambiwa wahame,huenda akufukuzae hakwambii toka.!!!!!!!!!

Article 0

$
0
0
ZAIDI YA WANAFUNZI LAKI NANE KUHITIMU DARASA LA SABA 2013 NCHINI KOTE.

Paper ni Kesho na Keshokutwa.


Hapa ni halmashauri ya wilaya ya Njombe ambapo wasimamizi  Mbalimbali wamefika kuchukua Mitihani ya Darasa la Saba itakayofanyika Kesho  septemba 11 na 12  Mwaka Huu.

Zaidi ya Wanafunzi Laki Nane Nchini Kote Wanatarajia Kuhitimu Elimu ya Darasa la Saba Mwaka Huu.

Mtandao huu Unawatakia Kila la Kheri na MTIHANI MWEMA Kwa wanafunzi hao.
Viewing all 2276 articles
Browse latest View live