
Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, aliwaeleza waandishi wa habari jijini hapa jana kuwa wathumiwa hao walikamatwa usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Kiombo, Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida.
Idadi hiyo ya meno ambayo thamani yake bado haijajulikana, inaonyesha kuwa jumla ya tembo 26 wameuawa na majangili katika maeneo ya Pori la Akiba la Rungwa na
Kizigo.
"Msako zaidi unaendelea kuwakamata watu wote waliohusika na mtandao wa mauaji ya tembo hao 26," alisema.
Hata hivyo, Waziri Nyalandu alisema majina ya watuhumiwa hao wa ujangili ambao wote ni Watanzania, yatatajwa baadaye, lakini alisema wanatarajiwa kufikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo.
Kwa hisani ya mjengwablog