TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LEO FEB 22,2014![]()

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Lakamata Pombe Kali Zilizopigwa Marufuku Na Serikali.
Mtu Mmoja Auawa Kwa Kupigwa Na Kundi La Wananchi Jijini Mbeya.
Mnamo
Tarehe 21.02.2014
Majira Ya
Saa 07:30hrs Asubuhi
Mtu Mmoja Asiyefahamika Jina Wala Makazi Yake, Jinsi Ya Kiume, Miaka Kati Ya 25-30 Alifariki Dunia Baada Ya Kufikishwa Hospitali Ya Rufaa Mbeya Kwa Matibabu Baada Ya Kupigwa Sehemu Mbalimbali Za Mwili Wake Na Kundi La Wananchi Walioamua Kujichukulia Sheria Mkononi Wakitumia Silaha Za Jadi Fimbo Na Mawe. Marehemu Alikamatwa Wakati Akivunja Duka Na Kuiba Vipodozi Mbalimbali Mali Ya
Daniel Mwanjala (40) Daktari
, Mkazi Wa Ghana Jijini Mbeya Tarehe
20.02.2014
Majira Ya
Saa 03:00hrs Usiku
Huko Sokomatola Kata Ya Maendeleo Na Tarafa Ya Sisimba Wilaya Ya Mbeya Mjini. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Jamii Kuacha Tabia Ya Kujichukulia Sheria Mkononi Kwani Ni Kinyume Na Sheria Na Badala Yake Wawafikishe Watuhumiwa Wanaowakamata Kwa Tuhuma Mbalimbali Katika Mamlaka Husika Ili Sheria Dhidi Yao Ichukuliwe.
Mtoto Mwenye Umri Wa Mwaka 01 Afariki Dunia Baada Ya Kutumbukia Kwenye Ndoo Ya Maji.
Mtoto Aliyefahamika Kwa Jina La
Beth Pakipo (01)
Mkazi Wa Bujera Alifariki Dunia Baada Ya Kutumbukia Kwenye Ndoo Iliyokuwa Na Maji Wakati Akicheza Na Watoto Wenzake Wenye Umri Kati Ya Miaka 02
–
03. Tukio Hilo Lilitokea Mnamo Tarehe
21.02.2013
Majira Ya
Saa 13:00hrs Mchana
Huko Kijiji Na Kata Ya Bujera Tarafa Ya Pakati Wilaya Ya Rungwe. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Wazazi/Walezi Kuwa Makini Kwa Kuweka Uangalizi Wa Kutosha Kwa Watoto Wao Ili Kuepuka Madhara Yanayoweza Kuepukika. Aidha Anatoa Wito Kwa Jamii Kufunika/Kufukia/Kuziba Mitaro/Visima/Mashimo Yaliyo Wazi Kwani Ni Hatari Kwa Watoto Hasa Katika Kipindi Hiki Cha Mvua Zinazoendelea Kunyesha Ili Kuepuka Madhara Yanayoweza Jitokeza.
Jeshi La Polisi Linamshikilia Mtu Mmoja Akiwa Na Bhangi Wilayani Kyela.
Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Linamshikilia Mtu Mmoja Aliyefahamika Kwa Jina La
Macrine Edson (32)
Mkazi Wa Ipinda Akiwa Na
Kete 122 Za Bhangi
Sawa Na
Uzito Wa Gram 610
. Mtuhumiwa Alikamatwa Katika Msako Uliofanyika Mnamo Tarehe
20.02.2014
Majira Ya
Saa 12:30hrs Mchana
Huko Katika Kijiji Na Kata Ya Ipinda Wilaya Ya Kyela. Mtuhumiwa Ni Muuzaji Wa Bhangi, Taratibu Za Kumfikisha Mahakamani Zinafanyika. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Jamii Kuacha Tabia Ya Kutumia Dawa Za Kulevya Kwani Ni Kinyume Cha Sheria Na Ni Hatari Kwa Afya Ya Mtumiaji.
Watu Watatu Wanashikiliwa Na Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Wakiwa Na Bhangi.
Watu Watatu Waliofahamika Kwa Majina Ya
1. Thabit Shaban (28) 2.
Michael Sigara (22)
Na
3. James Mwangande (22)
Wote Wakazi Wa Mkombwe Wanashikiliwa Na Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Baada Ya Kukamatwa Wakiwa Na
Bhangi Kete 14 Sawa Na Uzito Wa Gram 70
. Watuhumiwa Hao Walikamatwa Katika Msako Uliofanyika Mnamo Tarehe
21.02.2014
Majira Ya
Saa 16:00hrs Jioni
Huko Katika Kijiji Cha Mkombwe Kata Ya Ubaruku Tarafa Ya Rujewa Wilaya Ya Mbarali. Watuhumiwa Ni Wauzaji Na Watumiaji Wa Bhangi Hiyo, Taratibu Za Kuwafikisha Mahakamani Zinaendelea. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Jamii Kuacha Tabia Ya Kutumia Dawa Za Kulevya Kwani Ni Kinyume Cha Sheria Na Ni Hatari Kwa Afya Ya Mtumiaji.
Jeshi La Polisi Linamshikilia Mtu Mmoja Akiwa Na Bhangi Wilayani Momba.
Mtu Mmoja Aliyefahamika Kwa Jina La
Jesi Mwakangale (21)
Mkazi Wa Mtaa Wa Mwaka
–
Tunduma Anashikiliwa Na Jeshi La Polisi Baada Ya Kukamatwa Akiwa Na
Kete 171 Za Bhangi
Sawa Na
Uzito Wa Gram 855
. Mtuhumiwa Alikamatwa Katika Msako Ulioendeshwa Na Jeshi La Polisi Mnamo Tarehe
21.02.2014
Majira Ya
Saa 10:00hrs Asubuhi
Huko Katika Mtaa Wa Tukuyu, Kata Na Tarafa Ya Tunduma Wilaya Ya Momba. Mtuhumiwa Ni Muuzaji Na Mtumiaji Wa Bhangi, Taratibu Za Kumfikisha Mahakamani Zinaendelea. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Jamii Kuacha Tabia Ya Kutumia Dawa Za Kulevya Kwani Ni Kinyume Cha Sheria Na Ni Hatari Kwa Afya Ya Mtumiaji. Aidha Anaendelea Kutoa Wito Kwa Yeyote Mwenye Taarifa Za Mtu/Watu Wanaojihusisha Na Uuzaji/Ukulima Na Usambazaji Wa Dawa Za Kulevya Azitoe Kwa Jeshi La Polisi Ili Wakamatwe Na Hatua Za Kisheria Dhidi Yao Zichukuliwe.
Mtu Mmoja Anashikiliwa Na Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya Kwa Kosa La Kufanya Biashara Ya Kuuza Dawa Za Binadamu Bila Kibali.
Mfanyabiashara Mmoja Aliyefahamika Kwa Jina La
Awazi Mbalamwezi (29)
Mkazi Wa Msungwiji Anashikiliwa Na Jeshi La Polisi Baada Ya Kukamatwa Akiuza Dawa Za Binadamu Bila Kibali Katika Kibanda Chake Cha Biashara. Mtuhumiwa Alikamatwa Mnamo
Tarehe 21.02.2014
Majira Ya
Saa 16.45hrs Jioni
Katika Kitongoji Cha Msungwiji, Kijiji Cha Isangawana Wilaya Ya Chunya. Taratibu Za Kumfikisha Mtuhumiwa Mahakamani Zinafanyika. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala
Anatoa Wito Kwa Wafanyabiashara Kuacha Kufanya Biashara Bila Kibali Kwani Ni Kinyume Cha Sheria Na Ni Hatari Kwa Afya Ya Watumiaji.
................................................................................................................................................................................