Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 4

$
0
0
KESI YA WIZI WA KUTUMIA SILAHA YAENDELEA KUSIKILIZWA NJOMBE.

Na Gabriel Kilamlya Njombe

Mahakama ya Wilaya ya Njombe Hii Leo Imeendelea Kusikiliza Kesi ya Wizi wa Kutumia Silaha Inayowakabili  Stanley Kaduma Mwenye  Umri wa Miaka 30 na Shem Mgiliche Mwenye Umri wa Miaka 35 Wote Wakazi wa Ilunda Mkaoni Njombe.

Akisoma Hati ya Mashtaka  Mbele ya Hakimu wa Mahakama Hiyo Augustino Rwezile ,Mwendesha Mashtaka Atupakisye Mwakasitu Ameiambia Mahakama Kuwa   Washtakiwa Walitenda Kosa Hilo Oktoba Tatu Mwaka 201o Katika Kituo cha Kituo cha Kulelea Watoto Yatima Kilichopo Ilunda  Mkoani Njombe .

Imedaiwa Mahakamani Hapo na Mwendesha Mashtaka Mwakasitu Kuwa Washitakiwa Wakiwa na Bunduki Aina ya Shotgun Pomoja na Mapanga Walivamia Kituo cha Kulelea WatotoYatima na Kuiba Fedha Taslimu Shilingi Milioni Tisa Laki Tisa na
35 Elfu.

Washtakiwa Walipohojiwa Kutenda Kosa Hilo , Wamekana Kutenda Kosa Hilo Mbele ya Mahakama .

Hakimu wa Mahakama  Hiyo  Augustino Rwezile Ameahirisha Kesi Hiyo Hadi Septemba 18 Mwaka Huu Itakapo Sikilizwa Tena Huku Akiuagiza Upande wa Mashtaka Kuleta Mashahidi na Washtakiwa Wamerudishwa Lumande. 

Kwa Mara ya Kwanza Washtakiwa Hao Walifikishwa Katika Mahakama Hiyo Oktoba 27 Mwaka 2012 na Kusomewa Hati ya Mashtaka


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles