Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE HUENDA IKAFUTWA KWA KUTOFIKIA 80% YA UKUSANYAJI MAPATO HADI JUNI 30

$
0
0
Katibu tawala Wilaya ya Njombe Joseph Chota  atoa ripoti ya mwenendo wa Ukusanyaji mapato ya Ndani Katika Halmashauri tatu za Wilaya yake ya Njombe 

Na Gabriel Kilamlya NJOMBE

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Huenda Ikaenda Kufutwa Kama Serikali Kuu Ilivyoagiza Kuwa Kwa Halmashauri Itakayoshindwa Kukusanya Mapato ya Ndani Kwa Asilimia 80 Hadi Ifikapo Juni 30 Mwaka Huu Itafutwa Kutokana na Kufikia Takribani Asilimia 70 Pekee Hadi Sasa.

Taarifa Iliyotolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Njombe Joseph Chota Wakati Kituo Hiki Kilipofika 

Kupata Ripoti Hiyo Imeeleza Kuwa Katika Wilaya ya Njombe ni Halmashauri Moja Pekee ya Wilaya 

Ambayo Hadi Sasa Haijafikia Asilimia 80.

Aidha Amepongeza Jitihada Zilizofanywa Katika Halmashauri za Mji wa Makambako na Mji Njombe 

Kuvuka Agizo Hilo Kwa Mbinu Mbalimbali Licha ya Changamoto Kubwa Zilizokuwepo Huku Akisema 

Kumegwa Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Kuzalisha Halmashauri Nyingine Tatu za 

Wangin'ombe,Njombe Mji na Mji wa Makambako Ni Miongoni Mwa Sababu Zilizosababisha Kukwama 

Kufikia Kwa Asilimia Hizo.

Katika Hatua Nyingine Ameiagiza Halmashauri Hiyo Kuongeza ubunifu Katika Kuongeza Vyanzo 

Vipya Vya Mapato Pamoja na Wakusanyaji wa Mapato Hayo Kuhakikisha Wanaacha Visingizio Vya 

Mtandao Wakati wa Utoaji Risiti ya
Mfumo wa Mashine ya Kielektroniki.


Wakati wa Kuahirisha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11 Mjini Dodoma Hii Leo Waziri Mkuu Kassim 

Majaliwa Ameagiza Halmashauri Kuongeza Kasi Ukusanyaji Mapato Hayo Ikiwa ni Pamoja na Udhibiti 

wa Upotevu wa Mapato Hayo.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles