TAARIFA YA UCHUNGUZI WA UGONJWA WA UKUNGU WA VIAZI MVIRINGO MKOA WA NJOMBE

UTANGULIZI
Tarehe 18/02/2016 kituo kilipokea taarifa ya mlipuko wa ugonjwa wa kukauka viazi mviringo kutoka mkoa wa Njombe ukiomba tusaidie kubaini tatizo na kushauri jinsi ya kunusuru hali iliyotokea. Tarehe 9/03/2016, timu ya watafiti watano wakiongozwa na mratibu wa utafiti kanda ilifika mkoani Njombe kwa ajili ya uchunguzi wa tatizo lililoliripotiwa.Taarifa ya awali kutoka ofisi ya mkoa ilibainisha kuwa ugonjwa ulikuwa umeathiri hadi asilimia 90 ya mavuno kwenye baadhi ya halmashauri za wilaya. Halmashauri za wilaya zilizoathirika zaidi ni pamoja na Njombe Mji, Wanging’ombe, Ludewa na Makete.
UCHUNGUZI ULIVYOFANYIKA.
Uchunguzi ulifanyika kwa kutembelea baadhi ya mashamba yaliyoathirika, mahojiano na maafisa kilimo mkoa, wilaya, kata na vijiji na wakulima walioathirika pamoja na uchukuaji wa sampuli za viazi na majani yenye ugonjwa kwa uchunguzi wa maabara baada ya. Jumla ya wilaya mbili (Njombe Mji na Wanging’ombe) na vijiji sita vitatu kutoka kila wilaya vilitembelewa, Kisilo, Lugenge na Matola kwa upande Njombe Mji na Itulahumba, Igima na Ulembwe kwa upande wa Wanging’ombe.
MATOKEO YA UCHUNGUZI
3.1 Madhara ya Ugonjwa
Madhara ya ugonjwa yalikuwa makubwa kama yalivyojionyesha katika upungufu wa mavuno uliojitokeza kwa wakulima ambapo msimu uliopita walikuwa wanavuna kati ya gunia 40 hadi 60 ukilinganisha na 2 hadi10 ya msimu huu kwa ekari ambayo ni hasara ya karibu asilimia 94%.
Picha na.1: Moja kati ya mashamba yaliyoathirika na ukungu katika kijiji cha Utalingolo, Halmashauri ya Njombe Mji (Picha kwa hisani ya Kilumile-Afisa Kilimo).
3.2 Tatizo Halisi
Matokeo ya uchunguzi wa awali yameonyesha ugonjwa uliosababisha viazi kukauka ni ukungu unaojulikana kama ‘late blight’ ikichanganyika kidogo na ‘early blight’ kwa majina ya kitaalamu. Huu sio ugonjwa mpya bali ni ukungu uliozoeleka kwa misimu yote ambapo hushambulia viazi na nyanya lakini kwa msimu huu mlipuko wa ugonjwa uliochangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa kulikosababisha kuongezeka kwa mvua na joto kama ilivyothibitishwa na wataalamu wa kilimo, wakulima karibu wote tuliowatembelea na takwimu za hali ya hewa kutoka katika kituo cha Utafiti wa Kilimo,Igeri mkoani Njombe. Wakulima wengi walisema walikuwa wanasikia harufu kali kutoka shambani siku chache baada ya shamba kuathirika, hii ikiwa ni moja ya dalili kubwa ya shamba lililoshambuliwa na ukungu wa viazi mviringo .Sampuli za majani katika uchunguzi wa maabara pia zimeonyesha uwepo wa vimelea vya ukungu kama inavyoonekana katika picha namba 2(a&b).
B
A
![]()
![]()
B |
A |
Picha na. 2: Mbegu za vimelea vya ukungu kama vinavyooonekana katika darubini (x40) A. Ukungu wa mwanzo (Early blight) B. Ukungu wa mwisho (Late blight)
Sababu Zilizochangia Mlipuko wa Ugonjwa
Kuongezeka kwa Mvua
Ukilinganisha na misimu iliyopita (Jedwali na.1), msimu huu mvua zilikua nyingi na zilinyesha mfululizo hivyo kuvipa vimelea vya ukungu mazingira mazuri au rafiki ya kuzaliana, kukua na kusambaa. Wastani wa milimita 209.6 zilinyesha msimu huu kati ya Oktoba 2015 na Februari 2016 ukilinganisha na 166.28 za msimu wa 2014/15 na 158.12 za msimu wa 2013/14. Mbegu za ukungu husambaa kwa kuogelea hivyo uwepo wa mvua nyingi husaidia ugonjwa kusambaa kwa haraka.
Jedwali na.1: Takwimu za hali ya hewa za misimu mitatu 2013-2016 kuanzia Oktoba hadi Februari kutoka katika kituo cha hali ya hewa cha Utafiti wa kilimo Igeri, Njombe.
Msimu | Mwezi | Mvua(Kiasi katika mm) | Mvua(Siku) | Jotola juu | Jotola chini | Kiasicha unyevu | |
2013/2014 | Oct.Nov.Dec.Jan.FebWastani | 12.371.0273.7254.2179.4158.12 | 5823212115.6 | 22.519.021.119.920.120.52 | 10.210.512.011.511.911.22 | 888894919390.8 | |
2014/2015 | Oct.Nov.Dec.Jan.FebWastani | 23.931.8184.0323.9267.8166.28 | 6117272214.6 | 22.322.321.520.020.421.3 | 10.812.212.512.112.311.98 | 858692969691.0 | |
2015/2016 | Oct.Nov.Dec.Jan.FebWastani | 8.7209.0278.2261.9290.2209.6 | 21219221714.4 | 20.720.520.420.521.820.78 | 10.110.412.113.016.512.42 | 858890979791.4 | |