HUYU NDIYE MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE VALENTINO HONGORI AKIHUTUBIA MADIWANI NA WATUMISHI WA HALMASHAURI
MBUNGE WA JIMBO LA LUPEMBE JORAM HONGORI AKITOA NASAHA MBELE YA MADIWANI HAO
PICHA YA PAMOJA YA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA
Madiwani Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Wamemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri Hiyo
Kuhakikisha Watumishi Wote Wanaishi Kwenye Vituo Vyao Vya Kazi Wakiwemo Waratibu Elimu Na
Watendaji Wa Kata Na Kwamba Kwa Wasiyofanya Hivyo Wanatakiwa Kushushwa Wadhifa Wao Na
Kwenda Kufundisha Shuleni Kwa Waratibu Hao.
Wakizungumza Kwenye Mkutano Huo Wa Baraza La Madiwani Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya
Njombe Madiwani Hao Wamesema Shughuli Za Utekelezaji Wa Miradi Ya Vijiji Na Kata Kutokana Na
Watumishi Kuishi Mbali Na Vituo Vyao Vya Kazi Ambapo Wamesema Idadi Kubwa Ipo Kwa
Watendaji Wa Vijiji,Waratibu Elimu Na Watendaji Wa Kata.
Wamesema Kuwa Halmashauri Hiyo Imeshindwa Kufikia Lengo Ambalo Ilijiwekea La Kukusanya
Mapato Huku Majukumu Mengine Ya Ukamilishaji Wa Miradi Nayo Yakidaiwa Kushindwa
Kukamilika Pamoja Na Uharifu Kutokea Katika Maeneo Ya Vijiji Kutokana Na Walinzi Wa Amani
Kuwa Hawapo Maeneo Yao Ya Kazi.
Akizungumza Kwenye Hitimisho La Baraza La Madiwani Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya
Njombe Valentino Hongori Amesema Watendaji Na Waratibu Wanaoishi Mabili Na Mahala Pa Kazi
Mkurugenzi Anapaswa Kuchukua Hatua Za Kinidhamu Dhidi Yao Ikiwemo Kushushwa Vyeo Vyao
Kwa Watakao Kaidi Agizo Hilo.
Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Paul Malala Amesema Kuwa Tatizo Hilo Ambalo
Limelalamikiwa Na Madiwani Atakwenda Kufuatilia Na Majibu Atayatoa Kuanzia Mwezi Januari Na
Ameahidi Kuanza Kufuatilia Kwa Afisa Elimu Ili Kuhakikisha Waratibu Na Watendaji Wote Wanakaa
Kwenye Vituo Vyao Vya Kazi Na Atakayekiuka Hatua Kali Zitachukuliwa Dhidi Yao.