Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

MARAIS NA VIONGOZI WA MATAIFA MBALIMBALI WAWASILI TANZANIA KUSHUHUDIA UAPISHO WA DR.MAGUFULI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe (katikati chini) akimsubiria Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe (katikati juu kwenye ngazi) alipokuwa akiteremka kwenye Ndege, Rais Mugabe amewasili nchini kwaajili ya kuhudhuria Sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Waziri Membe akimpokea Rais Mugabe (mwenye Ua Mkononi) mara tu baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini pia anayeiwakilisha Tanzania nchini Botswana Mhe. Radhia Msuya (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Rais wa Botswana Mhe. Olale Eric Mothibi alipo wasili nchini kwaajili ya kushiriki Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Picha na Reginald Philip

Rais Mugabe akikagua Gwaride la Heshima.Rais Mugabe akiangalia kikundi cha wapiga Tarumbeta huku Waziri Membe akitoa ufafanuzi wa nyimbi iliyokuwa inachezwa.  

================================

 Mhe. Netumbo Nandi - Ndaitwah (wa pili kutoka kulia) akifurahia kikundi cha ngoma kilichopo mbele yao.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles