BARAZA LA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE LAVUNJWA RASMI LEO![]()
![]()
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba Akizungumza Katika Kikao Cha Kuvunja Baraza la Madiwani Hao Leo.
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Wakati Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Likivunjwa Hii Leo,Halmashauri Hiyo Imesema Imefikia Asilimia 91 ya Ukusanyaji Mapato Katika Kipindi Cha Miaka Mitano ya 2010/2015.
Akizungumza Wakati wa Kufungua Kikao Cha Kawaida Cha Baraza la Madiwani Kilichoambatana na Uvunjaji Baraza Hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Bwana Edwin Mwanzinga Amesema Kuwa Amesema Halmashauri Hiyo Katika Kipindi Cha Miaka ya Fedha ya 2010/2011 Hadi 2013/2014 .
Imefanikiwa Kukusanya Zaidi ya Shilingi Bilioni 4.1 Amesema Lengo Lilikuwa ni Kukusanya Kiasi Cha Shilingi Bilioni 4.5 Ambapo Kiasi Hicho Cha Shilingi Bilioni 4.1 Ambacho ni Sawa na Asilimia 91 Kimesaidia Kusogeza Mbele Shughuli Mbalimbali za
Maendeleo.
Pamoja na Mambo Mengine Lakini Mwanzinga Amesema Katika
Kipindi Hicho Chote Halmashauri Hiyo Imefanikiwa Kuandaa
Hesabu na Kubuni Vyanzo Vipya Vya Mapato Jambo Lililoifanya
Halmashauri Hiyo Kuendelea Kupata Hati Safi Katika Kipindi
Chote.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba
Wakati Akitoa Salaamu za Serikali Katika Baraza Hilo la
Mwisho Ametumia Fursa Hiyo Kuwapongeza Madiwani kwa
ushirikiano mkubwa walioutoa katika kutekeleza shughuli
mbalimbali za maendeleo katika kata zao na hasa katika
kutekeleza agizo la Rais la Ujenzi wa Maabara Tatu za
Sayansi Katika Kila Shule ya Sekondari.
Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Njombe
Limevunjwa Likiwa na Madiwani 19 Ambao 13 ni Wa Kata
Husika,viti maalum 6 na mmoja kutoka chama cha CHADEMA
kata ya njombe mjini Bwana Agrey Mtambo.
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba Akizungumza Katika Kikao Cha Kuvunja Baraza la Madiwani Hao Leo.
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Wakati Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Likivunjwa Hii Leo,Halmashauri Hiyo Imesema Imefikia Asilimia 91 ya Ukusanyaji Mapato Katika Kipindi Cha Miaka Mitano ya 2010/2015.
Akizungumza Wakati wa Kufungua Kikao Cha Kawaida Cha Baraza la Madiwani Kilichoambatana na Uvunjaji Baraza Hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Bwana Edwin Mwanzinga Amesema Kuwa Amesema Halmashauri Hiyo Katika Kipindi Cha Miaka ya Fedha ya 2010/2011 Hadi 2013/2014 .
Imefanikiwa Kukusanya Zaidi ya Shilingi Bilioni 4.1 Amesema Lengo Lilikuwa ni Kukusanya Kiasi Cha Shilingi Bilioni 4.5 Ambapo Kiasi Hicho Cha Shilingi Bilioni 4.1 Ambacho ni Sawa na Asilimia 91 Kimesaidia Kusogeza Mbele Shughuli Mbalimbali za
Maendeleo.
Pamoja na Mambo Mengine Lakini Mwanzinga Amesema Katika
Kipindi Hicho Chote Halmashauri Hiyo Imefanikiwa Kuandaa
Hesabu na Kubuni Vyanzo Vipya Vya Mapato Jambo Lililoifanya
Halmashauri Hiyo Kuendelea Kupata Hati Safi Katika Kipindi
Chote.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba
Wakati Akitoa Salaamu za Serikali Katika Baraza Hilo la
Mwisho Ametumia Fursa Hiyo Kuwapongeza Madiwani kwa
ushirikiano mkubwa walioutoa katika kutekeleza shughuli
mbalimbali za maendeleo katika kata zao na hasa katika
kutekeleza agizo la Rais la Ujenzi wa Maabara Tatu za
Sayansi Katika Kila Shule ya Sekondari.
Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Njombe
Limevunjwa Likiwa na Madiwani 19 Ambao 13 ni Wa Kata
Husika,viti maalum 6 na mmoja kutoka chama cha CHADEMA
kata ya njombe mjini Bwana Agrey Mtambo.