Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

DIWANI WA KATA YA UWEMBA EDWARD MWALONGO ATANGAZA RASMI NIA YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NJOMBE KUSINI[ccm]

$
0
0
Diwani wa Kata ya Uwemba Mheshimiwa Edward Mwalongo Akitangaza Nia Yake ya Kugombea Ubunge Jimbo la Njombe Kusini Kupitia Tiketi ya CCM
Baadhi ya Marafiki wa Mtia Nia Edward Mwalongo Walioshiriki Katika Zoezi Hilo Leo Mjini Njombe

Na Gabriel Kilamlya Njombe

Diwani wa kata ya uwemba ambaye ni Mkurugenzi wa taasisi ya Elimu ya Hagafilo leo ametangaza 

rasmi nia yake ya kutaka kugombea ubunge katika jimbo la Njombe kusini kupitia tiketi ya chama 

cha mapinduzi Ccm.

Akitangaza Nia Yake Hiyo na Vyombo vya Habari bila Kuwahusisha wananchi Bwana Mwalongo Amesema 

Licha ya Vipaumbele Vingi na Changamoto Nyingi Kuwepo katika jimbo hilo lakini lazima apiganie 

suala la elimu kwa nguvu zote.

Amesema endapo chama kitampitisha na wananchi wakamchagua kuwa mbunge wa jimbo hilo basi 

atapigania suala la miundombinu mbalimbali kama maji, barabara, umeme kwa
kuwa karibu zaidi 

wakati wa uwekaji vipaumbele Katika bajeti.


Akizungumzia suala la wabunge wengi kuwa na Mazoea ya kutelekeza majimbo yao mara baada ya 

kuchaguliwa amesema  yeye hawezi kuwa mbunge wa Christmas, Pasaka na mwaka mpya kwani hana 

makazi mengine yanayoweza kumuingizia pato Nje ya Njombe hivyo Hawezi kuwa kama wabunge hapo.

Akijibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari yaliyolenga juu  ya kuboresha na kukuza 

maendeleo katika Jimbo la Njombe kusini ikiwemo  ufinyu wa bajeti  kwa kila mwaka pamoja  na 

uchache wa fedha ya jimbo ambapo amesema ataendelea kupigania kadri atakavyoweza kwa kuvutia  na 

kuwekeza masuala ya kiutalii ndani ya Mkoa wa Njombe badala Ya  kuhama jimboni humo.

Pamoja na mambo mengine amesema  kinachopaswa ni kuwakaribisha kwa wingi wawekezaji katika mkoa 

wa Njombe  ikiwa ni pamoja na kuongeza fursa za kutosha za kiuwekezaji na kuzisimamia vizuri.

Hata hivyo amesema kwa kuwa mkoa wa njombe umekuwa na fursa nyingi za kujiingizia kipato hivyo 

suala la elimu kwa wananchi linahitajika zaidi ili kukuza pato la mkoa na wananchi kwa ujumla.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles