Kaimu mkuu wa Mkoa wa Njombe ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akielezea hali halisi ya utekelezaji wa shughuli za TASAF katika mkoa wa Njombe .
Meneja wa miundombinu mhandisi Elisifa kinasha akielezea madhumuni ya mkutano wa TASAF awamu ya tatu.
Meneja wa fedha Bw.Godwinne Mkisi akitoa mada juu ya uratibu wa kutuma fedha.
Afisa wa uratibu toka TASAF bw.Quintus Kassese akiwasilsha mada juu ya mpango wa kunusuru kaya masikini
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo akizindua mkutano wa kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu Mjini Njombe leo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw. Peter Ilomo (Hayupo pichani).
Mkurugenzi mtendaji wa TASAF akitoa maelezo ya utangulizi juu ya miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw.Peter Ilomo (Hayupo pichani).
Mtendaji Toka TASAF Beatrice Mbyallu akiwa na Baadhi ya Watendaji wa TASAF wakifuatilia kwa makini michango ya washiriki
Baadhi ya Watendaji wa TASAF wakiandaa mahitaji katika mkutano huo.
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji toka TASAF Wakiwemo wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi watendaji
nNa Gabriel Kilamlya Njombe
Wakazi katika Halmashauri 13 za Mikoa ya Njombe na Arusha Wanaanza Kunufaika na Mradi wa
Kupunguza Umaskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF utakaogharimu kiasi cha dola za
kimarekani milioni kumi na sita nukta nne kwa ufadhili wa OPEC awamu ya tatu.
Kaul Hiyo imetolewa Leo na Katibu Mkuu ofisi ya rais Ikulu bwana Peter Ilomo Wakati akizindua
rasmi utekelezaji wa mpango huo wa OPEC awamu ya tatu mjini Njombe na kuhudhuriwa na Wakuu wa
wilaya, wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi watendaji, wakuu wa Idara na watendaji wa TASAF
ambao watapata fursa ya kujengewa uwezo juu ya
utekelezaji wa mpango huo kwa muda wa siku mbili.
Kaya zitakazonufaika na miradi hiyo ni zile zilizobainishwa na kuandikishwa kwenye Mpango wa
Kunusuru Kaya Maskini katika Halmashauri zote za mkoa wa Njombe na Arusha.
Ilomo amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu pekee hivyo unapaswa
utekelezwe kwa kasi na umakini mkubwa ili kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo
yaliyokusudiwa.
Pamoja na mambo mengine,mkurugenzi mtendaji wa TASAF bw.Ladislaus Mwamanga pia ametumia fursa
hiyo kuwaonya watendaji watakaofanya kazi ya kuzibaini kaya masikini hususani katika maeneo
ambayo hayajafikiwa kuacha kuwaweka watu ambao watakuwa hawana sifa kwa kuwa tu ni ndugu,rafiki
au jamaa zao jambo ambalo halitofumbiwa macho hata kidogo.
Bw. Mwamanga amezitaja baadhi ya changamoto ambazo zinachangia kuwepo kwa malalamiko miongoni
mwa wananchi kuwa ni pamoja na kuchelewa kuanza kwa mradi huo hususani kwa kaya ambazo
zimeshafikiwa.
Miongoni mwa mambo yatakayofanyika katika miradi hiyo ni pamoja na kutoa ajira za muda mfupi
kwa walengwa,kuanzisha miradi endelevu ya ujasiliamal Pamoja na miradi ya elimu ya afya katika
jamii ambayo itatoa fursa ya kujiongezea kipato kwa wanufaika hao.
Hata hivyo jumla ya wakazi milioni 3.1 watanufaika na miradi hiyo mara baada ya kutambuliwa
kupitia mradi huo wa Awamu ya tatu katika mikoa hiyo miwili.
Meneja wa miundombinu mhandisi Elisifa kinasha akielezea madhumuni ya mkutano wa TASAF awamu ya tatu.
Meneja wa fedha Bw.Godwinne Mkisi akitoa mada juu ya uratibu wa kutuma fedha.
Afisa wa uratibu toka TASAF bw.Quintus Kassese akiwasilsha mada juu ya mpango wa kunusuru kaya masikini
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo akizindua mkutano wa kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu Mjini Njombe leo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw. Peter Ilomo (Hayupo pichani).
Mkurugenzi mtendaji wa TASAF akitoa maelezo ya utangulizi juu ya miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw.Peter Ilomo (Hayupo pichani).
Mtendaji Toka TASAF Beatrice Mbyallu akiwa na Baadhi ya Watendaji wa TASAF wakifuatilia kwa makini michango ya washiriki
Baadhi ya Watendaji wa TASAF wakiandaa mahitaji katika mkutano huo.
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji toka TASAF Wakiwemo wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi watendaji
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa kazi kutoka Halmashauri za mkoa wa Njombe.
Wakazi katika Halmashauri 13 za Mikoa ya Njombe na Arusha Wanaanza Kunufaika na Mradi wa
Kupunguza Umaskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF utakaogharimu kiasi cha dola za
kimarekani milioni kumi na sita nukta nne kwa ufadhili wa OPEC awamu ya tatu.
Kaul Hiyo imetolewa Leo na Katibu Mkuu ofisi ya rais Ikulu bwana Peter Ilomo Wakati akizindua
rasmi utekelezaji wa mpango huo wa OPEC awamu ya tatu mjini Njombe na kuhudhuriwa na Wakuu wa
wilaya, wenyeviti wa halmashauri, wakurugenzi watendaji, wakuu wa Idara na watendaji wa TASAF
ambao watapata fursa ya kujengewa uwezo juu ya
utekelezaji wa mpango huo kwa muda wa siku mbili.
Kaya zitakazonufaika na miradi hiyo ni zile zilizobainishwa na kuandikishwa kwenye Mpango wa
Kunusuru Kaya Maskini katika Halmashauri zote za mkoa wa Njombe na Arusha.
Ilomo amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu pekee hivyo unapaswa
utekelezwe kwa kasi na umakini mkubwa ili kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo
yaliyokusudiwa.
Pamoja na mambo mengine,mkurugenzi mtendaji wa TASAF bw.Ladislaus Mwamanga pia ametumia fursa
hiyo kuwaonya watendaji watakaofanya kazi ya kuzibaini kaya masikini hususani katika maeneo
ambayo hayajafikiwa kuacha kuwaweka watu ambao watakuwa hawana sifa kwa kuwa tu ni ndugu,rafiki
au jamaa zao jambo ambalo halitofumbiwa macho hata kidogo.
Bw. Mwamanga amezitaja baadhi ya changamoto ambazo zinachangia kuwepo kwa malalamiko miongoni
mwa wananchi kuwa ni pamoja na kuchelewa kuanza kwa mradi huo hususani kwa kaya ambazo
zimeshafikiwa.
Miongoni mwa mambo yatakayofanyika katika miradi hiyo ni pamoja na kutoa ajira za muda mfupi
kwa walengwa,kuanzisha miradi endelevu ya ujasiliamal Pamoja na miradi ya elimu ya afya katika
jamii ambayo itatoa fursa ya kujiongezea kipato kwa wanufaika hao.
Hata hivyo jumla ya wakazi milioni 3.1 watanufaika na miradi hiyo mara baada ya kutambuliwa
kupitia mradi huo wa Awamu ya tatu katika mikoa hiyo miwili.