Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276
↧

Article 0

$
0
0

  WATU WANNE WANASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA UVAMIZI WA KITUO CHA MAFUTA CHA ORYX MAKAMBAKO PAMOJA NA KUWAUA WALINZI WAWILI.


Focas Malengo Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe azungumza na www.gabrielkilamlya.blogspot.com
.....................................................................................................................
Siku Moja Baada ya Watu Wanaodaiwa Kuwa Majambazi Kuvamia Kituo Cha Mafuta Cha ORYX Makambako na Kuwaua Walinzi Wawili wa Kituo Hicho na Kumjeruhi Meneja wa Kituo Hicho,Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Linawashikilia Watu Wanne Kwa Madai ya Kuhusika na Tukio Hilo.

Hata Hivyo Jeshi la Polisi Halikuweza Kuweka Wazi Majina ya Watu Hao Kutokana na Sababu za Kiuepelelezi na Hivyo Kuwaomba Wananchi Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi Hilo Ili Kuweza Kuwabaini Watu Waliotenda Tukio Hilo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Njombe Focas Malengo Amesema Katika Tukio Hilo Pia Jeshi la Polisi Walifanikiwa Kuokota Silaha Moja Inayodaiwa Kuporwa na

Majambazi Hao.

Amesema Kutokana na Tukio Hilo Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Limeanzisha Msako Mkali Katika Miji ya Jirani Kwa Kushirikiana na Mikoa Hiyo.

Mnamo June 24 Mwaka Huu Majira ya Saa Kumi na Mbili na Nusu Asubuhi Watu Wanaodaiwa Kuwa Majambazi Walivamia Kituo Cha Mafuta ORYX Makambako na Kuwaua Kwa Risasi Walinzi wawili wa Kituo Hicho na Kupora Kiasi Cha Fedha zinazokisiwa kuwa ni kati ya shilingi Milioni tano au sita.

Mashuhuda wa Tukio Hilo walisema  kuwa majambazi hao  wawili  wakiwa na usafiri wa piki piki ambapo  walifika  katika  kituo hicho kwa ajili ya  kununua mafuta  ya Tsh 5000 na  wakati wakiendelea  kuhudumiwa ghafla  walianza  kuwashambulia walinzi kwa  risasi na  kuwaua walinzi  wawili na kumjeruhi meneja  wa  kituo  hicho.

Kaimu kamanda  wa  polisi mkoa  wa Njombe Focas Malengo  amethibitisha  kutokea kwa  tukio  hilo na  kuwataja  waliouwawa  kuwa ni Jonas Mpogole na Chesco Sanga ambao ni  walinzi wa kampuni ya ulinzi ya Makambako .

Mbali ya  kuwaua walinzi hao  wawili  pia majambazi hayo  yalimjeruhi  kwa risasi meneja  wa  kituo  hicho  Jonas Msenyi na kupora  fedha  zaidi ya Tsh milioni 5

Alisema  kuwa  jeshi la  polisi  linaendelea na msako  wa  kuwasaka majambazi  hayo ikiwa ni pamoja na  kuwaomba  wananchi  kutoa ushirikiano kwa  jeshi hilo la  polisi Licha ya kuwashikilia watu wanne wanaosadikiwa kuhusika katika Tukio Hilo.
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles