Katika Kuhakikisha Tatizo la walimu wa shule za Sekondari na Msingi linaendeleaa
kuatatuliwa, Mkoa wa Njombe Umepokea Walimu Zaidi ya Mia Nane Ambao
Wameanza Kuripoti Katika Vituo Vyao vya Kazi Tangu Hapo Juzi.
Akiongea na Kituo Hiki Afisa Elimu Mkoa wa Njombe Bw Said Kinyaga Nyasiro
Amesema Kuwa Kati ya Walimu Hao walopangwa katika Mkoa wa
Njombe ni walimu
831 Ambapo Walimu wa Masomo ya Sayansi ni 54 huku walimu wa sanaa ni walimu
ni 445 na walimu wengine ni wa cheti wakiwa 332 .
Katika Hatua Nyingine Afisa Elimu Huyo Amewashauri wadau wa Elimu Pamoja na
Wananchi Mkoani Njombe Kutoa Ushirikiano Wa Kutosha na Kutokuwakatisha
Molali Walimu Wapya waliopangiwa ambao wanatarajia Kuanza Kutoa Elimu Katika
Mkoa wa Njombe.
Aidha Afisa Elimu Huyo Amebainisha Kuwa Walimu 179 wanaratajia Kwenda Wilaya
Ya Makete,132 Wilaya ya Ludewa, 127 Wilaya ya Wanging'ombe na Wilaya ya Njombe
Walimu 393 Watakao Sambazwa Kwenye Halmashauri Zake.
Bw Nyasiro Ameongeza Idadi Hiyo ya Walimu imekuja wakati Mkoa wa Njombe Ikiwa
na Upungufu wa Walimu Zaidi ya Elfu Mbili Hivyo Kuwataka Walimu Hao wapya
Kuwasili Katika Vituo Walivyopangiwa Mapema Kama Sheria Inavyosema.
Ameongeza Kuwa Mapokezi Hayo ya Walimu Yanaenda Sanjari na Uhakiki wa Uhalali
wa Walimu Hao Kwa Kuachunguza Vyeti Vyao.