Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276
↧

Article 0

$
0
0
Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Bi.Esterina Kilasi Aliyefika Katika Mahakama Ya Wilaya ya Njombe kutolea Ushahidi Juu ya Kesi Inayomkabili Aliyekuwa Katibu Tawala Wilaya ya Njombe Evagrey Keiya

Na James Festo Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Esterina Kilasi Jana Ametolea Ushahidi Wake Mbele ya

Mahakama ya Wilaya ya Njombe Dhidi ya Kesi ya Manunuzi Hewa wa Magurudumu Matano na Betri

Mbili za Gari Vyoti Vikiwa na Thamani ya Shilingi Milioni 14 Inayomkabili Aliyekuwa Katibu Tawala

Wilaya ya  Njombe Evegray Keiya.

Akitoa Ushahidi Wake Mahakamani Hapo , Mkuu Huyo wa Wilaya ya Wanging'ombe  Ameiambia

Mahakama Kuwa Ofisi Yake  Pamoja na Aliyekuwa Akikaimu Ofisi ya  Katibu Tawala  Wilaya ya

Wanging'ombe  Waliagiziwa  Matairi Matano Aina ya Gunrub Kwa Ajili ya Gari Yake Lakini

Hakuwahi Kuyaona  Magurudumu Hayo  Katika Ofisi Yake .

Akitoa Ushahidi  Mahakamani Hapo Shahidi Namba Mbili Ambaye ni Afisa Manunuzi wa Mkoa wa

Njombe  Gaitan  Malio Lugenge  Ameiambai Mahakama Kuwa Alipokea Taarifa ya Ununuzi wa

Magurudumu Matano na Betri Mbili Aina ya N70 na Kusema Kuwa Betri Moja Liliwekwa Kwenye

Gari Lenye Namaba za Usajili STJ 6821 ya Katibu Tawala Mkoa wa Njombe .

Akiendelae Kutoa Ushahidi Mahakamani Hapo Shahidi Namba Mbili Gaitan  Malio Lugenge

Ameieleza Mahakamani Hapo  Kuwa Magurudumu Waliyoyapokea Yalikuwa Tofauti na Yale

Yaliyoagizwa Yanunuliwe Kwani Magurudumu Waliyoyapokea Yalikuwa ni Aina Ya Bridgestoni

Badala ya Gunrub.

Kwa Upande Wao Washtakaiwa Wakitetewa na Wakili Wao Hawakutakiwa Kujibu Chochote

Mara Baada Kusikiliza Utetezi wa Upande wa Mashtaka Hakimu wa Mahakama Hiyo John Kapokolo

Ameahirisha Kesi Hiyo Hadi Machi Tano Mwaka Huu Itakapo Sikilizwa Tena Mahakamani Hapo na

Washitakiwa Wameachiwa Kwa Dhamana.

Katika   Kesi  Nyingine  Afisa Tawala Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Njombe Anna Wiketye

Mwenye Umri wa Miaka 33 Mkazi wa  Mtaa wa Bomani  Mjini Njombe   Amefikishwa Mahakamani

Hapo Kujibu Shtaka Linalo Mkabili  La Kutoa  Ushahidi Wa Uongo Kinyume Na Kifungu Cha Sheria

Namba 102 Sura Ya Kwanza Na Kifungu Namba 104 Sura Ya 16 Cha Sheria Za Makosa ya Jinai 

Kanuni  Ya Adhabu Katika Kesi Inayomkabili  Aliyekuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe.

Akisoma Hati Ya Mashtaka Mahakamani Hapo Mwendesha Mashtaka Wa Serikali Bwana Riziki 

Matitu Amesema Kuwa  Novemba 18 Mwaka Jana Mshtakiwa Alifikishwa Mahakamani Hapo Ili

kutolea Ushahidi Wa Kesi Ya Bw.Bori Salunge Ally, Evegray  Keiya na Bw Ibrahim Konga   na kutoa

Ushahidi wa Uongo ulioufanya Upande Wa  Mashitaka Kumuondoa Katika Orodha  ya Mashahidi 

Kwenye Kesi ya Matumizi Mabaya ya Ofisi  na Kusababisha Hasara ya Shilingi Milioni Mbili za 

Wilaya Hiyo.

Kwa Upande Wake Mshitakiwa Huyo Akijibu Mashtaka Yanayomkabili Mahakamani Hapo Amesema

Alikubali Kutoa Maelezo  Kwa Maofisa wa Takukuru  na Kwamba Ushahidi Huo Aliutoa  Kutokana

na Mazingira Aliyokuwa Nayo Wakati Akihojiwa Katika Ofisi Hizo na Haukuwa Hiari Yake.

Hata Hivyo Hakimu wa Mahakama Hiyo  Ameahirisha Kesi Hiyo Hadi Machi Tano  Mwaka Huu na

Mshitakiwa Yuko Nje Kwa Dhamana. 
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles