Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 1

$
0
0

KATIBU MKUU WA Wizara ya VIWANDA NA BIASHARA ULED  MUSSA LEO AMEWATAKA MAOFISA BIASHARA KWENDA KWA WANANCHI NA SI KUBAKI MAOFISINI MKOANI NJOMBE

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Uled Mussa Aliyekaa Pamoja na Mmiliki wa Mtandao Huu Ngugu Gabriel Kilamlya Aliyechutama Pembeni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Uled Mussa Amewataka Maofisa 

wa Biashara Katika Halmashauri na Mikoa Mbalimbali Hapa Nchini 

Kuwatembelea Wananchi na Wakulima Vijijini Badala ya Kutumia Muda Mwingi 

Kukaa Maofisini.

Agizo Hilo Amelitoa Leo Wakati Akifanya Mazungumzo Maalumu  Alipotembelea 

Kituo Hiki  na Kupata Ufafanuzi Juu ya Mradi wa Muunganisho wa Ujasiliamali 

Vijijini MUVI Unaowahusisha Wakulima Mbalimbali wa Mazao ya Alizeti,Nyanya 

na Matunda Mkoani Njombe.

Bwana Mussa Amesema Kuwa Amebaini Kuwepo Kwa Maofisa Wengi wa 


Biashara Kushindwa Kuwafikia Wananchi na Wafanyabaishara Mbalimbaoli 

Kwenye Maeneo Yao Hali Inayosababisha Kuibuka Kwa Malalamiko Mbalimbali 

Toka Kwa Wafnyabaishara Hao.

Pamoja na Mambo Mengine Amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Njombe Capteni 

Mstaafu Asseri Msangi Kukaa na Wadau Mbalimbali Wa Kilimo Ili Kujadiliana 

Jinsi ya Kupanga Mazao Maalumu ya Kuyapa Kipaumbele Katika Mkoa wa 

Njombe Ili Kuyaunganisha Kwenye Mnyororo wa Thamani.

Mkoa wa Njombe ni Miongoni Mwa Mikoa Sita Inayotegemewa Kwa Uzalishaji 

wa Mazao Ya Chakula Hapa Nchini Kutoka Kusini Mwa Tanzania Huku 

Wakulima Wengi Hususani wa Mazao ya Biashara Vikiwemo Viazi Mviringo 

Wakiendelea Kulalamikia Tatizo la Vipimo Halisi Katika Uuzaji wa Mazao Yao.















Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Uled Mussa Kushoto Akiteta Jambo na Meneja wa Kituo Cha Redio Uplands Fm Njombe Mara Baada ya Kufanya Mazungumzo Redioni Hapo. Leo













Msafara wa Katibu Mkuu Huyo Ukiondoka Katika Kituo Cha Redio Uplands Fm Njombe Majira ya Jioni ya Leo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276