Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 2

$
0
0

WANANCHI  WA KIJIJI CHA ITULAHUMBA WAAHIRISHA SHUGHULI ZAO KWA AJILI YA KUMNG'OA MWENYEKI WA KIJIJI CHAO.
 AFISA TAARAFA YA MDANDU BENSON WANDERAGE AKIWA KWENYE MKUTANO WA HADHA AMBAO ULIKUSUDIA KUWAKATAA VIONGOZI WA KIJIJI AMBAO NI MWENYEKITI NA MTENDAJI ALIYEHAMISHIWA KIJIJINI HAPO



 DIWANI WA KATA YA MDANDU BI ANNA UPENDO GOMBELA AKIONGEA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA ITULAHUMBA KUHUSIANA NA MGOGORO WA KUWAONDOA VIONGOZI HAO






 WAJUMBE NA VIONGOZI WA SERIKALI YA KATA NA KIJIJI CHA ITULAHUMBA


 AFISA MTENDAJI WA KATA YA MDANDU BWANA  TIMOTH FUTE AKIZUNGUMZA NA WANANCHI JUU YA NAMNA ALIVYOHAMISHWA MTENDAJI HUYO TOKA KIJIJI CHA ITAMBO KWENDA KIJIJI CHA ITULAHUMBA HUKU ALIKWISHA KUTUHUMIWA NA WANANCHI KWA UBADHILIFU WA MALI ZA KIJIJI
 MIONGONI MWA WANANCHI WA KIJIJI CHA ITULAHUMBA WAKIHOJI JUU YA KUPELEKEWA MTENDAJI HUYO




 WANANCHI WAKIWASIKILIZA VIONGOZI WA KATA NA TAARAFA YA MDANDU WILAYANI WANGING'OMBE
 HII NI OFISI YA KIJIJI CHA ITULAHUMBA



 HUyU NI MWENYEKITI ALIYEKAIMISHWA BWANA SHAIBU MAHEGELE  BAADA YA WANANCHI KUMFUKUZA MWENYEKITI WA ZAMANI BWANA HOSEA MPOSOLA

HUYU NI MWENYEKITI WA KIJIJI BWANA HOSEA MPOSOLA ALIYEFUKUZWA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA ITULAHUMBA WAKISEMA HAWANA IMANI NAE

  Na  Michael Ngilangwa
 
Hatimae sakata la wananchi wa kijiji cha Itulahumba la kuwakataa viongozi

limeingia sura mpya baada ya wananchi hao kumufukuza mwenyekiti wao na

kumuchagua mwenyekiti wa muda huku wakimuomba mkurugenzi kumuondoa afisa

mtendaji ambae amepelekwa hivi karibuni kusimamia maendeleo ya kijiji hicho.

Wakiongea mbele ya viongozi wa kata na taarafa ya Mdandu wananchi hao

wameelezea sababu za kumkataa mwenyekiti wa  kijiji hicho bwana Hosea Mposola

kwa kuruhusu afisa mtendaji aliyekuwepo bwana Method Mligo kuhamia kijiji cha

Itambo  bila kusoma hesabu za mapato na matumizi,kuruhusu afisa mtendaji mpya

kuhamia katika kijiji hicho pasipo wananchi kufahamishwa uwepo wake jambo

lililopelekea wananchi kutokuwa na imani na mwenyekiti huyo.

Kuhusu afisa mtendaji aliehamishiwa katika kijiji hicho akitokea kijiji cha Itambo

 bwana Batista Msemwa wananchi hao wamesema kuwa hawamuhitaji

mtendaji huyo kutokana na wananchi wa kijiji cha Itambo kumkataa kutokana na kutuhumiwa kuhusika na   ubadhilifu wa mali za kijiji cha Itambo na kwamba serikali  imekuwa na tabia ya kuwahamishia vijiji vingine watumishi wanaotuhumiwa na ubadhilifu wa mali za wananchi ili waendelee na ufujaji wa mali za wananchi.

Akizungumza kwenye mkutano  wa hadhara afisa taarafa ya Mdandu bwana Benson

Wanderage amesema kufuatia kuteuliwa kwa mwenyekiti wa muda wananchi

wanatakiwa kuonesha ushirikiano katika kutekeleza miradi ya kijiji hicho huku

akisema kuwa serikali ya kata itakwenda kumuagiza afisa mtendaji aliyehamishwa

arudi kijijini hapo ili asome  taarifa ya hesabu za mapato za matumizi.

Diwani wa kata ya Mdandu bi Anna Upendo Gombela amesema  amewapongeza wananchi kwa  mahudhurio ya wananchi hao na kwamba  lengo la kuwakutanisha wananchi hao ni kutatua mgogoro uliokuwepo baina ya viongozi na wananchi  wa kutokuwa na imani na uongozi wa kijiji  akiwemo mwenyekiti huku akisema wajumbe wa  serikali ya kijiji wameridhia kufanya uteuzi wa mwenyekiti wa muda ambae anakubalika na wananchi wote.

Afisa mtendaji wa kata ya Mdandu bwana Timoth Fute amesema kuwa ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe tayari imechukua  hatua za kumuandikia barua yakwenda kusoma hesabu za mapato na matumizi ya kijiji cha Itulahumba   mtendaji huyo pindi atakapo pona kwani kwa sasa amelazwa katika hospitali ya Kibena ambapo ameahidi kumsimamia ili kuhakikisha anakwenda kusoma taarifa za mapato na matumizi ya kijiji hicho ndipo  aweze kahama.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles