NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI ATEMBELEA KARAKANA YA RELI MJINI MOROGORO.

Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akiongea na vibarua walioajiriwa na kampuni ya SMH/Rail kutoka nchini Malaysia, asubuhi alipofanya ziara kwenye karakana ya Reli mkoani Morogoro kuangalia maendeleo ya uundwaji upya wa Vichwa vya Treni vya Shirika la Reli Tanzania(TRL). Naibu Waziri huyo ameuagiza uongozi wa kampuni hiyo kuhakikisha kuwa vibarua hao wanapewa mikataba kama watafanya kazi zaidi ya miezi mitatu kama sheria za kazi zinavyowataka.
Naibu Waziri wa Uchukuzi akiongea na Naibu Mtendaji Mkuu, Uendeshaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Mhandisi Paschal Mafikiri (wa kwanza kushoto), wakati alipotembelea Karakana ya Reli Mkoani Morogoro, leo asubuhi kuangalia maendeleo ya undwaji upya wa vichwa vya treni. Kichwa cha kwanza kinategemea kukamilika mwanzoni mwa Mwezi wa Disemba 2013.
CREDIT michuziblog