Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 20

$
0
0

POLISI NJOMBE WAKAA NA BODABODA KUJADILI HALI YA KUTISHA ILIYOIBUKA DHIDI YAO.





 BODABODA ZIKIWA ZIMEPAKIWA WAKATI WAMILIKI WAKE WAKIWA NDANI YA UKUMBI WA POLISI NJOMBE LEO

 WAMILIKI NA MADEREVA BODABODA WAKIINGIA NDANI YA UKUMBI WA POLISI NJOMBE KWENYE KIKAO NA POLISI KILICHO LENGA KUJADILIA SUALA LA KUPUNGUZA AJALI NA MATUKIO YA UHARIFU WA KUIBIWA PIKIPIKI NA MAUWAJI YANAYOFANYWA NA MAJAMBAZI MKOANI NJOMBE
 AFISA USALAMA WA BARABARANI MKOA WA NJOMBE MARO CHACHA AKIWAELEZA MADREVA HAO LENGO LA KUWAITISHA WAMILIKI NA MADEREVA WA BODABODA HIZO



 
Siku Kadhaa zilizopita Madereva wa Bodaboda waliingiwa na hali ya wasiwasi kutokana na matukio kadhaa yaliyotokea Mkoani Njombe dhidi yao na hivyo kuhatarisha usalama wa kazi zao.
 
Madereva hao wameonekana kuingiwa na hofu hiyo Ikiwa ni Wiki Moja tu Kupita Tangu Dereva Mwenzao wa Bodaboda Wa kituo cha Eneo la Sangamela Mjini Njombe Kutekwa na kuuawa Kinyama na Watu Wanaosadikika Kuwa ni Majambazi Ambapo Mtu mmoja Aliyekodi Pikipiki Kwa Kijana Huyo Ndiye Anasadikika Kusababisha Mauaji ya Dereva Huyo.

Sanjali na Hilo Lakini Pia Hivi Karibuni Kijana Mmoja Ambaye Hakujulikana alikutwa ametekwa na kutupwa Kwenye Maeneo ya Kata ya Njombe Mjini Ambaye Inasadikika Kuwa naye Alikuwa Dereva wa bodaboda.

Kutokana na matukio Hayo Madereva wa Bodaboda Mjini Njombe Wameingiwa na Hofu na Kuanza Kufikiria Mbinu Mbalimbali za Kuweza Kujilinda Bila Kupata Majibu ya Haraka.

Hivyo Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani Limelazimika Kuwaita na Kujadili Namna ya Kuimarisha Ulinzi Katika Biashara zao.

Picha na Michael Ngilangwa.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles