Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe Fulgency Ngonyani akiongea na mtandao huu ofisini
Na Prosper Mfugale Njombe
Jeshi la polisi mkoani Njombe linawashikilia watu watatu kwa kuhusika na matukio mawili Tofauti likiwemo la kutaka kuiba Transformer mali ya kampuni ya Tanesko katika kituo cha makambako Njombe
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la polisi kwa vyombo vya habari ina sema kuwa tukio la kwanza limetokea Augost 20 mwaka huu majira ya saa nne katika kijiji cha Ilunda ambapo
jeshi la polisi linawashikilia Imrani Sulemani miaka 40 na Beatus Urasa miaka 40 wakazi wa dar es laam kwa tuhuma za wizi wa tranfoma
Taarifa hiyo imesema kuwa jeshi la polisi lilipata taarifa ktoka kwa msamaria mwema na kisha kuweka mtego katika eneo la
transfoma hiyo mpaka lilipofanikiw kuwa tia mbaroni wakatti watuhumiwa wakati wakijiandaa kuiba na baaba ya kupekuliwa walikutwa na spana katika eneo la tukio Na katika tukio jingine jeshi la polisi linamshikilia Wainfrida wilomo mkazi wa kijiji cha kifanya mwenye umri wa miaka 20 kwa tuhuma za kumtumbukiza kwenye choo mtoto wa kiume mwenye umri wa miezi saba baada ya kujifungua nyumbani kwake
Jeshi la polisi linaendelea kumshikilia mtuhumiwa na kiini cha tukio hilo kinaendelea kuchunguzwa