Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

MIKOA YA NJOMBE NA IRINGA YAPEWA TUZO KWA KUFIKIA 98% YA UTOAJI WA VYETI VYA KUZALIWA

$
0
0



 WAZIRI WA MAMBO YA KATIBA NA SHERIA HARISON MWAKYEMBE BAADA YA KUWASILI MKOA WA NJOMBE KATIKA ENEO LA UKUMBI WA CHUO CHA MAENDELEO NJOMBE MJINI AKISALIMIANA NA WAKUU WA WILAYA ,WAKURUGENZI NA WATALAAMU MBALIMBALI WA MIKOA YA NJOMBE NA IRINGA


Na Michael  Ngilangwa  NJOMBE

Waziri wa  Katiba na Sheria Dokta Harison Mwakyembe leo  amekabidhi Tuzo Katika Halmashauri  na mikoa ya Njombe na Iringa ambayo imepata asilimia 98 Kwa  kuongoza katika zoezi la usajili wa watoto wenye umri chini ya miaka mitano   ulioendeshwa chini ya  Wakala  wa Usajiri, Ufilisi na Udhamini RITA.

Waziri Mwakyembe Amekabidhi Tuzo  Hizo kwa Halmashauri za Mkoa wa Njombe Na Iringa  baada ya kuongoza katika zoezi hilo la usajili wa vyeti vya kuzaliwa  na kupongeza kwa hamasa  iliyofanyika kwa mikoa hiyo ambayo miaka michache iliyopita   maendeleo  ya Usajili yalikuwa Duni ambapo  Njombe ilikuwa asilimia nane  na sasa  imefikia asilimia 98.

Waziri Mwakyembe Amesema Mikoa ya Njombe Na Iringa Imechangia kuijengea misingi imara ya maendeleo  ya Nchi  na kusema kuwa nchi yoyote ili ifanikiwe lazima iwe na takwimu sahahi za wakazi wake  na kupanga mipango  mbalimbali ya maendeleo ya kuanzisha Viwanda katika kuelekea Uchumi wa Kati wa Nchi ya Tanzania.

Amesema  Mikoa Mingine ya Tanzania Inapaswa Kutembelea Mikoa ya Njombe na Iringa Ili Kujifunza namna ilivyofanikiwa  katika kutekeleza zoezi la kuhamasisha wananchi  kupeleka watoto wao kuwasajili  na kusema jitihada hizo Zinatakiwa Kuendelee kufanyika hata kwa mikoa mingine kufikia asilimia walizopata  mikoa ya Njombe na Iringa.

Akisoma Taarifa Fupi Mbele ya Mgeni Rasmi Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Harison Mwakyembe ,Kaimu Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa  usajiri,Ufilisi  na Udhamini RITA Bi. Emmy Hudson  amesema Mkoa wa Njombe Na Iringa imeweza kuvuka malengo ya kusajili na kuwapa vyeti vya kuzaliwa  watoto wenye umri chini ya miaka mitano  Ambapo RITA Imeamua kupongeza mikoa iliyofanya vizuri Ili kuwa mfano kwa Mikoa mingine.

Kwa Upande Wao Wakuu wa Mikoa ya Njombe Na Iringa  Christopha Ole Sendeka na Amina Masenza Wameshukuru kwa kupewa zawadi hizo na kusema mpango wa kusajili watoto ulianza mwezi Decemba  22 ,2016   zikitolewa kwenye ofisi za watendaji wa kata na vituo vya tiba za mama  na mtoto  nakwamba  usajili huo sasa utakuwa ni agenda ya kudumu Na kulishukuru shirika la Unisef kwa kuwa mdau katika zoezi hilo.




 WAZIRI WA MAMBO YA KATIBA NA SHERIA HARISON MWAKYEMBE AKIWA UKUMBINI
 MKUU WA MKOA WA NJOMBE CHRISTOPHA OLE SENDEKA










 MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles