Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI ya mkoa wa Iringa imetekeleza agizo la Rais Dr John Magufuli kwa kukabidhi jumla ya madawati 21,304 kwa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri zote tano za mkoa huo .
Mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza akikabidhi mgao wa madawati hayo kwa wakurugenzi wa Halmashauri hizo leo zoezi lililofanyika kwenye karakana na chuo cha ufundi stadi VETA , alisema kuwa utekelezaji wa agizo hilo umefanikiwa kutokana na mwitikio mzuri wa wananchi wa mkoa huo na wadau mbali mbali wa maendeleo ambao kwa umoja wao wamesaidia zoezi hilo kukamilika .
Alisema kuwa Rais Dr Magufuli alitoa agizo kwa wakuu wote wa mikoa nchini kuhakikisha wanafunzi wote wanakaa katika madawati ifikapo leo Juni 30 mwaka huu na kuwa kutokana na agizo hilo alilazimika kuwashirikisha wakuu wake wa wilaya na wadau mbali mbali wakiwemo wananchi mmoja mmoja na kila mmoja kwa uwezo wake aliweza kuchangia madawati hadi kufanikisha zoezi hilo.
Mkuu huyo alisema kwa Halmashauri za mkoa wa Iringa zimetengeneza madawati kupitia bajeti zake na wadau waliopo kwenye Halmashauri husika na kuwa hadi sasa mkoa umetekeleza kutengeneza madawati hayo 21,304 wakati madawati 3665 huku madawati 8,163 kwa ajili ya shule za msingi wakati madawati 1,264 ya shule za sekondari yanaendelea kutengenezwa katika karakana mbali mbali na fedha kwa ajili ya matengenezo hayo tayari zimelipwa .
Hivyo alisema madawati yanayoendelea kutengenezwa yanatarajiwa kukamilika July 15 mwaka huu kwani yamechelewa kukamilika kutokana na wakandarasi wanaotumika kutengeneza madawati hayo kuwa na kazi nyingi .
Bi Masenza alisema kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na wadau mbali mbali imeweza kutengeneza madawati 700 kwa lengo la kuunga mkono jitihada za Halmashauri za kumaliza tatizo la madawati mapema ,ambayo yamegawiwa katika Halmashauri tano za mkoa wa Iringa ambazo ni Iringa Manispaa madawati 200, Mji Mafinga madawati 100 ,Halmashauri ya Iringa madawati 100 ,halmashaur i ya Mufindi madawati 100 na Kilolo madawati 100
Wakati madawati 308 yanaendelea kutengenezwa katika karakana ya VETA pindi yatakapokamilika yatafikisha idadi ya madawati 1,008 jumla ya fedha ambazo zimetumika kutengeneza madawati hayo 1,008 ni milioni 50,400,000 na baada ya madawati yote kukamilika kutengenezwa mkoa wa Iringa hautakuwa na upungufu wa madawati kwa wanafunzi zaidi ya kuwa na ziada ya madawati .
Mkoa wa Iringa una jumla ya shule za msingi 478 na shule za sekondari 107zinazomilikiwa na serikali na mkoa huo ulikuwa na upungufu wa madawati 29,347 ikiwa ni madawati 26,046 ya shule za Msingi na madawati 3301 kwa shule za sekondari. |