Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (katikati)
akizungumza na Machifu wa kisukuma kwenye kituo cha Utamaduni Bujora,
kulia pichani ni Jaji Mstaafu Mark Bomani na kushoto ni Chifu Charles
Kafipa wa Bukumbi mkoani Mwanza
akizungumza na Machifu wa kisukuma kwenye kituo cha Utamaduni Bujora,
kulia pichani ni Jaji Mstaafu Mark Bomani na kushoto ni Chifu Charles
Kafipa wa Bukumbi mkoani Mwanza
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amesimikwa uchifu wa kisukuma mara baada ya kutembelea kituo cha utamaduni wa kisukuma cha Bujora.
Katika tuzo hiyo ya watemi wa kisukuma ambayo risala yake imeandikwa na kusainiwa na Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma Mtemi CM. Dotto Itale, wamemtakia heri na kumuomba mwenyezi mungu amsaidie kufanya kazi zake vizuri na kumtunukia cheo cha Manju Mkuu kiongozi wa ngoma kubwa mwenye kughani umati wote ukaitikia, na kumpa jina la Sangija ambalo linaunganisha Mamanju wote.