msimamizi wa uchaguzi mkoa wanjombe akitolea ufafanuzi juu ya namna uchaguzi utakavyoendeshwa ,kuanzia kampeni ambazo zinaendelea ,upigaji kura na kutangazwa matokeo | Na Gabriel Kilamlya NJOMBE |
|
|
| Imeelezwa kuwa matumizi mazuri na sahihi ya kalamu kwa wanahabari katika mchakato wa Uchaguzi mkuu Nchini ndio njia pekee itakayoliweka Taifa sehemu salama katika zoezi hilo muhimu . |
|
|
| Kauli hiyo imetolewa na kaimu katibu tawala Mkoa wa Njombe bwana Gideon Mwinami wakati akizungumza katika mkutano wa wadau wa habari Mkoani Njombe ulioandaliwa na chama cha Waandishi wa habari mkoa huo(Njombe Press Club) chini ya ufadhili wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Nchini Tanzania UTPC. |
|
|
| Bwana Mwinami amesema kuwa kuzingatiwa kwa kanuni, sheria na miiko ya uandishi wa habari katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu kutasaidia zoezi hilo liweze kwenda vizuri kwani hakutakuwa na uchochezi wala upendeleo kwa baadhi ya vyama vya siasa. |
|
|
| Hilmar Danda ni mratibu wa uchaguzi na mwanasheria toka ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Njombe ambaye Amesema hadi sasa maandalizi ya vifaa vitakavyotumika siku ya kupiga kura yameshakamilika na bado mambo machache ambayo Hume yenyewe bado haijatoa muongozo. |
|
|
| Aidha bwana Danda amesema kuwa tume haikotayari kuona amani inatoweka katika mchakato huo eti kutokana na chama fulani kutaka kubebwa. |
|
|
| Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Njombe bwana John Temu Amesema jeshi la polisi limeimarisha na litaendelea kuimarisha ulinzi na usalama katika zoezi hilo ikiwa ni pamoja na kuwek | ka doria katika kila eneo na vituo vya uchaguzi siku ya uchaguzi. |
|
|
| Taarifa ya chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe iliyosomwa na katibu wa chama hicho bwana Hamis Kassapa imevitaka vyombo vinavyohusika na zoezi hilo hususani Jeshi la polisi na tume ya Taifa ya uchaguzi kutenda haki katika mchakato huo ili kuepusha lawama dhidi ya vyombo vya habari. |
|
|
| Baadhi ya wanasiasa walioshiriki mkutano huo akiwemo mgombea ubunge jimbo la Njombe kusini kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema bwana Emmanuel Masonga na mwakilishi wa chama cha mapinduzi ccm Anold Mtewele wametumia fursa hiyo kuvitaka vyombo vya habari kutenda haki katika kampeni hadi uchaguzi mkuu ili kuepusha adha inayoweza kujitokeza. |