HALI ILIVYOKUWA NYUMBANI KWA PROFESA JAY, ULIPO MSIBA WA MAMA YAKE.
Mama mzazi wa Msanii Profesa Jay amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kugongwa na gari maeneo ya mbezi juu jijini Dar alikokuwa anaishi na mwanae.
Habari zinadai kwamba, marehemu Bi. Rosemary Manjara Haule aligongwa na gari akiwa anavuka barabara kuelekea dukani mida ya saa mbili na kwamba baada ya kugongwa wasamaria wema walimkimbiza hospitali ya Tumbi kwa kutumia bajaji ambako mauti ilimkuta huko .