
Serikali ya Sudan Kusini imekataa kusaini mkataba uliotarajiwa kuleta amani na kumaliza mapigano yaliyodumu nchini humo kwa zaidi ya miezi ishirini.
Serikali imeomba kuongezewa siku kumi na tano zaidi kushauriana juu ya mapendekezo hayo.
Waziri kutoka Uingereza anayesimamia maswala ya Afrika ameitaka serikali ya Sudan Kusini kutia sahihi mkataba huo
haraka iwezekanavyo.
Amesema kuwa watu hawafai kusheherekea hadi pale rais Kiir atakapotia sahihi mkataba huo.