Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike
Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Kimewataka Wanachama Wapya Ambao Wamechukua Kadi za Uanachama Baada ya Julai 15 Mwaka Huu Kutojisumbua Kwenda Kwenye Matawi Yao Kupiga Kura za Maoni Kuwapata Wabunge na Madiwani Watakaopeperusha Bendera ya Chama Hicho Katika Uchaguzi Mkuu.
Kauli Hiyo Imetolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike Kufuatia Kuwepo Kwa Taarifa za Kusambazwa Kwa Kadi za Uanachama Hivi Karibuni Baada ya Kuanza Kwa Kampeni za Kura za Maoni Katika Nafasi ya Diwani na Ubunge.
Mpagike Amesema Kwa Mujibu wa Chama Hicho Anayetoa Kadi Hizo ni Katibu wa Tawi na Si Mtu Mwingine na Hivyo Kama Kuna Mwanachama Amepata Kadi Mitaani Badala ya Viongozi Hao Basi Wajue Kuwa Hakuna Jina Lao Kwenye Ofisi Hizo na Kwamba Siku ya Kupiga Kura Hapo Kesho Wanatakiwa Kufika na Kadi ya Uanachama na Kitambulisho cha
Mpiga Kura.
Kwa Upande wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Njombe Kimeelezea Juu ya Mchakato wa Kupiga Kura Kuwapata Madiwani Watakaopeperusha Bendera ya Chama Hicho Katika Kura za Maoni na Kwamba Zoezi Hilo Litaanza Agosti 7 Mwaka Huu.
Akizungumzia Suala Hilo Katibu wa Chama Hicho Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa Amesema Kuwa Ratiba Hiyo Itakwenda Kuanzia Agosti 7 Hadi 12 Baada ya Kutolewa Kwa Ratiba na CHADEMA Makao Makuu Jijini Dar es Salaam.
Hata Hivyo Ametoa Wito Kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Kuangazia Katika Vyama Vyote Vya Siasa Katika Chaguzi Hizo Kutokana na Kuwepo Kwa Mianya ya Rushwa
Huku Maafisa Hao Kuangazia Zaidi Katika Chama Tawala Pekee.
Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Kimewataka Wanachama Wapya Ambao Wamechukua Kadi za Uanachama Baada ya Julai 15 Mwaka Huu Kutojisumbua Kwenda Kwenye Matawi Yao Kupiga Kura za Maoni Kuwapata Wabunge na Madiwani Watakaopeperusha Bendera ya Chama Hicho Katika Uchaguzi Mkuu.
Kauli Hiyo Imetolewa na Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike Kufuatia Kuwepo Kwa Taarifa za Kusambazwa Kwa Kadi za Uanachama Hivi Karibuni Baada ya Kuanza Kwa Kampeni za Kura za Maoni Katika Nafasi ya Diwani na Ubunge.
Mpagike Amesema Kwa Mujibu wa Chama Hicho Anayetoa Kadi Hizo ni Katibu wa Tawi na Si Mtu Mwingine na Hivyo Kama Kuna Mwanachama Amepata Kadi Mitaani Badala ya Viongozi Hao Basi Wajue Kuwa Hakuna Jina Lao Kwenye Ofisi Hizo na Kwamba Siku ya Kupiga Kura Hapo Kesho Wanatakiwa Kufika na Kadi ya Uanachama na Kitambulisho cha
Mpiga Kura.
Kwa Upande wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Njombe Kimeelezea Juu ya Mchakato wa Kupiga Kura Kuwapata Madiwani Watakaopeperusha Bendera ya Chama Hicho Katika Kura za Maoni na Kwamba Zoezi Hilo Litaanza Agosti 7 Mwaka Huu.
Akizungumzia Suala Hilo Katibu wa Chama Hicho Mkoa wa Njombe Alatanga Nyagawa Amesema Kuwa Ratiba Hiyo Itakwenda Kuanzia Agosti 7 Hadi 12 Baada ya Kutolewa Kwa Ratiba na CHADEMA Makao Makuu Jijini Dar es Salaam.
Hata Hivyo Ametoa Wito Kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Kuangazia Katika Vyama Vyote Vya Siasa Katika Chaguzi Hizo Kutokana na Kuwepo Kwa Mianya ya Rushwa
Huku Maafisa Hao Kuangazia Zaidi Katika Chama Tawala Pekee.