
Prof. Mwandosya amesema jambo la Rais kulihutubia bunge ni suala muhimu sana hivyo si vyema mbunge ama kundi fulani la wabunge kuwepo nje ya bunge wakati Rais atakapokuwa analihutubia bunge.
Kauli hiyo ya Prof. Mwandosya ameitoa leo Bungeni, ikiwa siku chache tu kupita tangu Mkuu wa kambi ya Upinzani bungeni ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (uKAWA) Mhe. Freeman Mbowe kusema wabunge wa umoja huo
hawatarejea tena bungeni.