Mwenyekiti wa Vijana CCM Mkoa wa Njombe Bwana Imani Fute Akitoa Taarifa ya Wadhamini Zaidi ya Elfu Kumi Waliojitokeza Kumdhamini Lowasa Mkoani Njombe
Lowasa akionesha majina ya wadhamini waliomdhamini Mkoani Njombe baada ya kupokea toka kwa katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Cremence Mponji Aliyesimama
Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike Akimkaribisha Edward Lowasa Ili Awashukuru Wadhamini Wake na Wananchi Mkoani Njombe
Edward Lowasa Akizungumza na Maelfu ya Wananchi Waliojitokeza Katika Kumdhamini
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowasa Leo Amewasili Mkoani Njombe Kuomba Wadhamini Katika Mchakato wa Kugombea Nafasi ya Urais Mwezi Oktoba 25 Mwaka Huu.
Akizungumza na Wanachama Waliojitokeza Kumdhamini Mbunge Huyo Pamoja na Wananchi Mbalimbali Mjini Njombe Lowasa Amesema Endapo Watanzania Watamchagua Kuongoza Taifa la Tanzania Hatokubali Kuendelea Kuona Watanzania Wanaendelea Kuwa Masikini Ili Hali Taifa Lina Rasilimali za Kutosha.
Amesema Endapo Atapata Ridhaa Hiyo Basi Ataendesha Nchi Kwa Mchakamchaka na Kwa Atakayeona Anashindwa Kuendana Naye Basi Anatakiwa Kupisha Mapema Kwa Lengo la Kuwakomboa Watanzania.
Suala la Serikali Kununua Mahindi ya Wakulima Kwa Mkopo Amesema Hataki Kulisikia Tena Endapo Atashinda Katika Uchaguzi Huo na Kwamba Kama Serikali Itakopa Mazao Hayo Kwa Wakulima Basi Walipwa na Riba.
Imani Fute ni Mwenyekiti wa Vijana CCM Mkoa wa Njombe Ambaye Amesema Katika Mkoa wa Njombe Zaidi ya Wanachama Elfu Kumi Wamejitokeza Kumdhamini Lowasa Katika Kinyang'anyiro Hicho.
Kwa Mujibu wa Katibu wa CCM Wilaya ya Njombe Bwana Clemence Mponji Amesema Hadi Sasa Jumla ya Watia Nia 11 Katika Nafasi ya Urais Ndio Waliofika Kuomba Wadhamini Katika Mkoa wa Njombe.