Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Muuaji wa kanisani Charleston ashtakiwa

$
0
0
Mshukiwa wa mauaji ya kanisani nchini Marekani ameshtakiwa na mashtaka tisa ya mauaji
Mshukiwa wa mauaji ya watu tisa katika kanisa la kihistoria la Kiafrika katika mji wa Charleston ameshtakiwa na mashtaka tisa ya mauaji pamoja na shtaka moja la kumiliki silaha.

Mshukiwa Dylan Roof mwenye umri wa miaka 21,Amefikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani kupitia teknolojia ya video.

Polisi Wameyachukulia mauaji hayo katika kanisa la Emanuel AME siku ya jumatano usiku katika mji wa kusini mwa Carolina kama uhalifu wa chuki.

Amekamatwa siku iliofuata yapata maili 200 kutoka mji wa Carolina kaskazini kabla ya kusafirishwa na kurudishwa mjini Charleston.

Gavana wa jimbo la Carolina Kusini Nikki Haley amesema kuwa Roof anapaswa kupewa adhabu ya kifo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles