Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

KATIBU WA CHADEMA MKOA WA NJOMBE ALATANGA NYAGAWA ATANGAZA RASMI NIA YAKE YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NJOMBE KUSINI LEO

$
0
0
Mwanasiasa Mkongwe Alatanga Nyagawa Ambaye ni Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Njombe Akitangaza Rasmi Nia Yake ya Kugombea Ubunge Jimbo la Njombe Kusini Leo





Na Gabriel Kilamlya Njombe

Katibu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Njombe Bwana Alatanga Nyagawa Ametangaza Rasmi Nia Yake ya Kutaka Kugombea Ubunge Katika Jimbo la Njombe Kusini Kupitia Tiketi ya Chama Hicho.

Akizungumza na Vyombo Vya Habari Mara Baada ya Kutangaza Nia Yake Hiyo Alatanga Amesema Endapo Wakazi wa Njombe Watamchagua Kuwa Mbunge Ndani ya Jimbo Hilo Basi Atatumia Uwezo wa Kiushawishi  Alionao Katika Kuhakikisha Anawapata Wawekezaji wa Kuwekeza Katika Sekta Mbalimbali Mkoani  Njombe.

Alatanga Amesema Tatizo la Soko Kwa Wakulima wa Chai Ndani ya Mkoa wa Njombe Linashindwa 

Kupatiwa Ufumbuzi Kutokana na Usimamizi Dini wa Viongozi Waliopo Madarakani na
Kusababisha Adha 

Kubwa Kwa Wakulima.

Aidha Amesema Ridhaa ya Wananchi Kumchagua Kuwa Kiongozi Katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba 

Mwaka Huuu Endapo Chama Kitampitisha Basi Atahakikisha Anawatafuta Wawekezaji wa Nje na Ndani 

Ambao Watakuja Kujenga Viwanda Vya Kutosha Vya Chai Mkoani Hapa.


Akizugumzia Suala Sugu la Maji Katika Mji wa Njombe na Maeneo Mengine Hapa Nchini Alatanga 

Amesema Uzembe wa Baadhi ya Viongozi Waliopo Madarakani Ndio Chanzo Kikubwa Kinachokwamisha 

Kupatikana Kwa Maji ya Uhakika Katika Maeneo Mbalimbali.


Pamoja na Mambo Mengine Lakini Pia Amesema Suala la Ajira Kwa Vijana Litapewa Kipaumbele Zaidi 

Endapo Atachaguliwa Kwa Kuwaunganisha Pamoja na Kubuni Mambo ya Kufanya Badala ya Kubaki Bila 

Kazi Yoyote.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles