![]() | |
Mwili wa mgonjwa wa Ebola ukitolewa Wodini huku Liberia picha na maktaba |
Taarifa ambazo bado kuthibitishwa na wizara ya afya zinadai kuwa mgonjwa huyo alikuwa amwelazwa wodi namba 8 katika Hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa wa Iringa na baada ya kifo chake chenye shaka ya ebola vipimo vimechukuliwa na kupelwekwa kwa mkemia mkuu wa serikali ili kuweza kutoa majibu sahihi .
Mbali ya vipimo hivyo kuchukuliwa tayari ndugu wa mgonjwa huyo wanadaiwa kuteketeza nguo zake kwa moto kwa hofu ya kuambukizwa ugonjwa huo hatari na hadi sasa mwili wa marehemu huyo upo katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.
Mtandao wa www.matukiodaima.co.tz usiku wa Jana umetinga katika hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa wa Iringa na kupata taarifa za awali kutoka wodi 8 kuwa ni kweli kuna mgonjwa ametiliwa shaka na uchunguzi unaendelea na hadi kesho majibu yatapatikana .
Kwa hisani ya francisgodwin.blogspot