Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 0

$
0
0
 MWANAJESHI MARINO MBEYELA AZIKWA NJOMBE LEO

Wananchi wa mitaa ya Idundilanga Mjini Njombe wameshauliwa

kuimarisha ulinzi na usalaama katika maeneo yao ili kuhakikisha

uharifu wa mali unaofanyika kwa nyakati tofauti usiku na mchana

na baadhi ya watu wanaosadikika kuwa ni wezi  unatokomezwa.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa mtaa wa Idundilanga bwana

Augustino Mgeni wakati akitoa salaamu za serikali katika mazishi

ya aliyekuwa mwanajeshi Wa jesh la

wananchi Tanzania JWTZ Marino

Benedict Mbeyela yaliofanyika Jana kwenye makaburi ya Igominyi

Mjini Njombe.

Bwana Mgeni amesema kufuatia kukithili kwa uharifu unaofanywa na

baadhi ya watu, wananchi wanatakiwa kuonesha ushirikiano katika

kuwafichua wanaojihusisha na matendo hayo na kwamba uongozi wa

mtaa huo unatarajia kufanya msako muda wowote wa kuwabaini

waharifu.

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa Mtaa wa Idundilanga Mashaka

Lulambo amehimiza wananchi kujitokeza kuchangia michango

kwaajili ya ujenzi mbalimbali ambao unaendelea katika mtaa huo

na kwamba wanafunzi wa shule ya sekondari Joseph Mbeyela

wamekosa vyumba vya madarasa vya kutosha jambo linalolazimu

kuhimiza ujenzi huo.

Amesema kuwa kwa watakaoshindwa kuwasilisha michango hiyo kwa

wakati hatua kali za kisheria zitaanza kuchukuliwa na kwamba

kila mwananchi anatakiwa kuchangia shilingi elfu sita ili

kukamilisha ujenzi unaoendelea katika mitaa ya kata ya Njombe

mjini.

Akisoma Ibada ya mazishi ya marehemu Marino Benedict Mbeyela

ambaye enzi za uhai wake ametumikia jeshi la Wananchi wa

Tanzania JWTZ Kwa kipindi cha miaka thelathini Na nne Katekista

wa kanisa Katholiki Kigango cha Njombe Mjini Kelvin Myamba

amesema kuwa wakristo wanapaswa kumtumikia Mungu siku zote ikiwa

ni pamoja na kuungama dhambi zao.

Muwakilishi wa jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ Akisoma

taarifa fupi ya marehemu akawambia wananchi waliohudhulia

mazishi hayo namna walivyokuwa wakifanya kazi na marehemu kwamba wameshirikiana vizuri hadi alipokuja kuchukuliwa na mwenyezi Mungu.


kwa hisani ya michaelngilangwa blog

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles