Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276
↧

MTENDAJI WA KIJIJI MAJI SHINGONI IMALINYI

$
0
0

AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA IMALINYI ATAKIWA KUKABIDHI OFISI KESHO JUMATANO 18 JUNE KUTOKANA NA TUHUMA ZA KUVUJA MALI ZA KIJIJI





huyu ni afisa mtendaji wa kijiji cha Imalinyi Milton Mgobasa ambae amekataliwa na wananchi   na kupewa uhamisho na hapa anawasomea wananchi hesabu za mapato na matumizi ndipo akabidhi ofisi ya kijiji hicho.

Wananchi wa kijiji cha Imalinyi Wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe wamemsamehe afisa mtendaji wa kijiji hicho bwana Milton Mgobasa mapungufu yaliojitokeza katika taarifa yake ya hesabu za mapato na matumizi ambayo hayajasomwa kwa wananchi kwa takribani  mwaka mmoja na kuwataka watendaji wengine kuwa makini na utendaji wao kazi.

Wakiongea kwenye mkutano wa hadhara wananchi hao wamesema kuwa kutokana na uongozi wa kijiji hicho kuonesha mapungufu katika taarifa zao za hesabu za mapato na matumizi   wamemuomba mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Wnging'ombe kuagiza wakaguzi  wa vitabu  vya watendaji wa vijiji kila baada ya miezi mitatu  ili kubaini wa watendaji   wasiyo wadilifu kazini.

Aidha wananchi hao wameitupia lawama ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa kile kilichoelezwa na afisa mtendaji wa kijiji hicho Milton Mgobasa  kwamba   ofisi ya mkurugenzi haina vitabu  vya stakabadhi za  michango ya maendeleo ya vijiji  jambo ambalo diwani wa kata hiyo bwana Enock Kiswaga amekanusha hoja hizo za kukosekana vitabu.
WANANCHI WA KIJIJI CHA IMALINYI WAKISIKILIZA MAPATO NA MATUMIZI YA KIJIJI HICHO


MWENYEKITI WA KIJIJI CHA IMALINYI ADAM CHENGULA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI


RISITI FEKI ALIZOKUWA AKIZITUMIA AFISA MTENDAJI HUYO NA HIZO NDIZO ZILIZO MUONDOA KIJIJINI HAPO
DIWANI WA KATA YA IMALINYI ENOCK KISWAGA AKIKANUSHA HOJA YA KUKOSEKANA KWA VITABU VYA STAKABADHI ZA VIJIJI  AMBAZO VIONGOZI WA VIJIJI WALIKUWA WAKIJITETEA KWAMBA OFISI YA MKURUGENZI HAINA VITABU VYA STAKABAZI HIZO



MGANGA WA ZAHANATI YA IMALINYI AKITOA MATANGAZO JUU YA KUPATIWA VITAMBULISHO  VYA MATIBABU BURE KWA WAZEE.
 
Na  Michael Ngilangwa Wanging'ombe

Wananchi wa kijiji cha Imalinyi Wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe wamemsamehe afisa mtendaji wa kijiji hicho bwana Milton Mgobasa mapungufu yaliojitokeza katika taarifa yake ya hesabu za mapato na matumizi ambayo hayajasomwa kwa wananchi kwa takribani  mwaka mmoja na kuwataka watendaji wengine kuwa makini na utendaji wao kazi.


Wakiongea kwenye mkutano wa hadhara wananchi hao wamesema kuwa kutokana na uongozi wa kijiji hicho kuonesha mapungufu katika taarifa zao za hesabu za mapato na matumizi   wamemuomba mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Wnging'ombe kuagiza wakaguzi  wa vitabu  vya watendaji wa vijiji kila baada ya miezi mitatu  ili kubaini wa watendaji   wasiyo wadilifu kazini.

Aidha wananchi hao wameitupia lawama ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo kwa kile kilichoelezwa na afisa mtendaji wa kijiji hicho Milton Mgobasa  kwamba   ofisi ya mkurugenzi haina vitabu  vya stakabadhi za  michango ya maendeleo ya vijiji  jambo ambalo diwani wa kata hiyo bwana Enock Kiswaga amekanusha hoja hizo za kukosekana vitabu.

Akizungumza wakati wa kusoma hesabu ya taarifa ya mapato na matumizi afisa mtendaji wa kijiji cha Imalinyi ambae amepata uhamisho baada ya wananchi kumkataa Milton Mgobasa amesema kuwa kukosekana kwa vitabu vya stakabadhi za michango ya maendeleo ya miradi ya wananchi  imesababisha  kununua vitabu ambavyo halmashauri haijaidhinisha ili wananchi waendelee kuchangia  miradi  pasipo kutambua kuwa ni kinyume na sheria.

Diwani wa kata ya Imalinyi Enock Kiswaga amesema   marufuku kwa maafisa watendaji kununua kitabu mahala anapojua yeye na kuanza kukitumia pasipo halmashauri kuidhinisha huku akisema  utetezi wa mwenyekiti wa kijiji hicho Adam Chengula  na afisa mtendaji huyo kwamba halmashauri haina vitabu si wa kweli kwani vitabu halmashauri vipo vya kutosha  na kwamba ni uzembe wa kuvifuata huku akitumia fursa hiyo kumtambulisha afisa mtendaji  aliyehamia badala ya  aliyekuwepo awali.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho  bwana Adamu Chengula akiwa kwenye mkutano huo alikuwa mstali wa mbele kuwambia wananchi kuwa halmashauri  ya Wilaya ya Wanging'ombe haina vitabu vya stakabadhi kutokana na taarifa alizodai kuzipata kwa afisa taarafa wa Imalinyi jambo ambalo diwani wa kata hiyo alikanusha kauli hiyo.
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles