MGOMBEA UBUNGE WA CCM GOFREY MGIMWA AENDELEA NA KAMPENI ZAKE TOSAMAGANGA .![]()
Mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga,Godfrey Mgimwa akiwa emebebwa juu na Wananchi na wanachama wa CCM wakielekea kwenye eneo la Mkutano wa hadhara wa kampeni.

Wakazi wa Kalenga A,wakifurahia jambo wakati wa mkutano wa kampeni za Ubunge kupitia CCM zilizofanyika leo.

Wakifuatilia kwa makini
Makamu Mwenyekiti (BARA) wa CCM,Ndugu Philip Mangula akihutubia kwenye kumtano wa hadhara wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga,mapema leo jioni kwenye Kata ya Kalenga A-Iringa vijijini.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga,kupitia tiketi ya CCM,Ndugu Godfrey Mgimwa akiwahutubia wakazi wa kata ya Kalenga A mapema leo jioni kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu akipokea kadi ya Chadema iliyorudishwa na Ndugu Said Omary Mbilinyi ambaye amerudi CCM baada ya kutoelewa sera na siasa za Chadema.


Msanii maarufu Tanzania mwenye vipaji vya kuigiza ,kucheza na kuimba Dokii akiimba na kucheza pamoja na Diwani wa Viti Maalum na Mwenyekiti wa UWT Iringa Vijijini Ndugu Shakira Kiwanga wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge za CCM kwenye kitongoji cha Tosamaganga.

Wananchi wakifurahia jambo

Wanafuatilia kwa makini

Usijali kijana wetu,tayari ushindi ni wako-

Sister Paula Msambwa mwenye umri wa miaka 73 na aliyewahi kuwa mwalimu wa Marehemu William Mgimwa kuanzia darasa la kwanza mpaka la nne ambapo alimfundisha somo la hisabati, amesema amefarijika kumuona mtoto wa mwanafunzi wake akigombea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Kalenga.pichani shoto ni Mgombea Ubunge wa jimbo hilo,kwa tiketi ya CCM,Ndugu Godfrey Mgimwa akisikiliza kwa makini

Godfrey Mgimwa akipewa mkono wa kila la kheri na Sister Paula,kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu

Wanachama wa CCM wakiserebuka na Mgombea wao wakielekea kwenye kata ya Kalenga A


Wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla wakiserebuka na Mgombea wao wakielekea kwenye kata ya Kalenga A kwa ajili ya mkutano wa kampeni uliofanyika jioni ya leo.