
MBEYA
Mtu Mmoja Aliyefahamika Kwa Jina La William Henard Mwenye Umri wa Miaka 48 Mkazi Wa Magogo
Aliuawa Kwa Kukatwa Panga Kichwani Na Mbozyo Samson Mwenye Umri wa Miaka 40 Mkazi Wa Magogo.
Tukio Hilo Lilitokea Mnamo Tarehe 22.02.2014 Majira Ya Saa 23:30hrs Usiku Huko Katika Kitongoji Cha
Magogo Kijiji Cha Ileya, Kata Ya Ifwenkenya Tarafa Ya Songwe Wilaya Ya Chunya.
Chanzo Cha Mauaji Ni Wivu Wa Kimapenzi Kumgombea Regina Charles Mwenye Umri wa Miaka 39 Mkazi
Wa Magogo.
Mtuhumiwa Amekamatwa Na Taratibu Za Kisheria Zinaendelea Dhidi Yake.
Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala Anatoa Wito Kwa Jamii Kutatua Migogoro Yao Ya Kimapenzi Kwa Njia Ya Kukaa Meza Ya
Mazungumzo.
Aidha Anatoa Wito Kwa Wapenzi Kuwa Waaminifu Kwa Kuwa Na Mpenzi Mmoja Ili Kuepuka Madhara
Yanayoweza Kuepukika.
Katika Tukio Jingine Mwendesha Pikipiki Aliyefahamika Kwa Jina La Danken Mwampashi Mwenye Umri wa
Miaka 42 Mkazi Wa Old Vwawa Alifariki Dunia Baada Ya Kugongwa Na Gari Lenye Namba Za Usajili It
6860 Aina Ya Toyota Corola Lililokuwa Likiendeshwa Na Muulu Muulu Mwenye Umri wa Miaka 37 Raia Na
Mkazi Wa Ndola Nchini Zambia
Tukio Hilo Lilitokea Mnamo Tarehe 23.02.2014 Majira Ya Saa 09:00hrs Asubuhi Katika Barabara Ya
Mbeya/Tunduma Kijiji Cha Hanseketwa, Kata Ya Vwawa, Tarafa Ya Vwawa Wilaya Ya Mbozi.
Chanzo Cha Ajali Ni Mwendo Kasi Wa Mpanda Pikipiki Baada Ya Kuingia Barabara Kuu Bila Kuchukua
Tahadhali na Kwamba Mwili Wa Marehemu Umehifadhiwa Katika Hospitali Ya Serikali Ya Wilaya Ya Mbozi.
Dereva Amekamatwa. Kaimu Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishina Msaidizi Wa Polisi
Robert Mayala Anatoa Wito Kwa Madereva Kuwa Makini Wanapotumia Vyombo Vya Moto Kwa
Kufuata/Kuzingatia Sheria Na Alama Za Usalama Barabarani Ili Kuepuka Ajali Zinazoweza Kuepukika.
Aidha Anatoa Wito Kwa Watumiaji Wengine Wa Barabara Kuzingatia Alama Za Usalama Barabarani Ili
Kuepuka Ajali Zinazoweza Kuepukika.
..............................................................................................................................................................................