Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 14

$
0
0
MMOJA MBARONI KWA MAUAJI  LUDEWA NJOMBE 
 Kamanda wa Polis Mkoa wa Njombe SACP Fulgence  Ngonyani 

 Na  Michael  Ngilangwa

Jeshi la polisi mkoa wa Njombe linamshikilia mkazi mmoja wa kijiji cha Madunda Wilayani Ludewa  Samson  Haule kwa tuhuma za kuhusika na mauaji  yaliotokea katika kata ya Mawengi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe Fulgence Ngonyani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa huyo anashikiliwa kwa mahojiano kutokana na tuhuma za kuhusika katika mauaji yaliomkuta Anna Solomon mwenye umri wa miaka 58 mkazi wa kijiji cha madunda Wilayani Ludewa.

Kamanda Ngonyani amesema kuwa    tukio hilo limetokea mnamo february 11 mwaka huu majira ya saa kumi jioni ambapo marehemu akiwa amelala nyumbani kwake alivamiwa na

watu wasiyofahamika kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kufariki dunia.

Amesema kuwa chanzo cha tukio hilo kinasadikika ni mgogoro wa mashamba ambao walikuwa wakigombania ambapo uchunguzi dhidi ya tukio hilo bado unaendelea na utakapokamilika mshtakiwa atafikishwa mahakamani.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276