Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 1

$
0
0
SHIRIKA LA KILIMO LA NADO NJOMBE KUFANYA TAMASHA LA JUKWAA LA WAKULIMA MAY 30 NA 31 IGWACHANYA.
Mkurugenzi wa shirika la maendeleo ya kilimo Mkoani Njombe NADDO Bwana John Wihallah akielezea Juu ya Tamasha la Jukwa la wakulima wilayani Wanging'ombe Mwezi huu.

Na Gabriel Kilamlya.

Katika kukabiliana na Changamoto za Wakulima katika Sekta ya Kilimo

Nchini Shirika la Maendeleo ya Kilimo Mkoani Njombe NADDO linatarajia

kufanya maonesho ya Jukwaa la Wakulima Wilayani Wanging'ombe Ikiwa

ni Maandalizi ya Kuwapata  Wakulima Bora Watakaoshiriki Maonesho ya

NaneNane  Mwaka Huu Mkoani Mbeya

Akizungumza na Kituo hiki juu ya Jukwaa Hilo mkurugenzi wa Shirika la

NADDO Bwana John Wihallah amesema Takribani Wakulima Elfu Tano
waliopata Mafunzo ya Mashamba Darasa Mwaka Huu Watashiriki Katika
Jukwaa Hilo litakalofanyika Kwa siku mbili kuanzia mei 30 na 31 Mwaka

huu katika Ofisi za Shirika Hilo Zilizopo kwenye Makao makuu ya Wilaya

ya Wanging'ombe Kule Igwachanya.

Amesema kuwa jukwaa hilo litawapa Fursa wakulima katika Kutambua

changamoto zinazo wakabili ili kuangalia namna ya kuzipatia Ufumbuzi

kwa kushirikiana na Serikali.

Katika Hatua Nyingine Bwana Wihallah ameeleza kuwa kwa sasa tayari

wakulima wameanza kunufaika na mafunzo ya Mashamba Darasa

waliyokuwa wakiyapata pamoja na kujifunza Ujasiliamali ambao  wamesha

anza kwa kutengeneza Sabuni,Batiki pamoja na ufugaji Kuku.

Hata hivyo katika kuwainua kiuchumi kutokana na Shughuli zao za Kilimo

amesema kuwa Shirika hilo tayari limefanikiwa kusajiri Taasisi ya Kifedha

ya SACCOS Itakayowasaidia kutumia katika ukopaji wa Fedha za miradi

mbalimbali.................................................................


Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles