Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

WAUGUZI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE WAITAKA SERIKALI KULIPA FEDHA ZA LIKIZO KABLA YA KWENDA LIKIZO

$
0
0



 WAUGUZI WAKIWA KWENYE MAANDAMANO KUTOKEA HOSPITALI YA TANWAT KUELEKEA CHUO CHA WAUGUZI KIBENA 








 MGENI RASMI KATIBU TAWALA MSAIDIZI GIDEON MWINAMI AKIPOKEA MAANDAMANO HAYO

 WAUGUZI WANAWASHA MISHUMAA YA ISHARA YA UPENDO



Zaidi Ya Wauguzi 200  Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe   Wameungana Na Wauguzi Wengine  Kuadhimisha Siku  Ya Wauguzi Duniani Kote  Ambapo  Katika Kuadhimisha Siku Hiyo  Wamefanikiwa Kufikisha  Changamoto  Mbalimbali Ambazo Zimekuwa Zikiwakabili  Wauguzi Wakati Wa Kutekeleza Majukumu Yao Ikiwemo Kutopatiwa Mafao Ya  Kustaafu Kutoka Mashirika Ya Hifadhi Ya Taifa Ya Jamii.

Akizungumza Kwenye Maadhimisho Hayo Kwa Niaba Ya Katibu Tawala Mkoa Wa Njombe Jackson Saitabau,Katibu Tawala Msaidizi  Gideon Mwinami  Ametaka  Wauguzi Kuitumia Siku Hiyo Kwaajili Ya Kukumbushana  Utekelezaji Wa Majukumu Yao Kwa  Uadilifu Na Kufuata  Misingi Ya Maadili  Ya Utendaji Kazi Kwenye Vituo Vyao.

Kuhusu  Malalamiko Ya Wauguzi  Kutopandishwa Vyeo Na Kuongezewa Mishahara Pindi Wanapotoka Masomoni  Katibu Msaidizi Huyo Mwinami  Ameahidi Kuzifikisha  Changamoto Hizo Kwa  Mkurugenzi  Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Ili Kutatua  Zile Zilizo Chini Ya Uwezo Wake Huku Akitaka Jamii Kuwathamini Wauguzi  Hao  Kwa Kuonesha Ushirikiano  Wakati Wa  Kutekeleza Majukumu Yao.

Rustika Mtemba Ni Mwenyekiti Wa  Chama Cha Wauguzi  Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  TANNA  Ambaye Ametaka Serikali Kuwafikilia Swala La Kuwafanyia Mabadiliko Ya Kupandishwa Vyeo Na Mishahara  Wauguzi Wanapotoka Masomoni  Huku Akitupia Lawama  Mifuko Ya Taifa  Ya Hifadhi Ya Jamii Ikiwemo NSSF  Kwa Kushindwa Kutoa Mafao Yao Kwa Wakati.

Katika Risala Ya Wauguzi  Kwa Mgeni Rasmi Iliyosomwa Na  Dativa Mwinuka Imeeleza   Kuwepo Kwa Changamoto Ya Wauguzi Kutopewa Sale Za Kazi,Kutolipwa Fedha Za Likizo Kwa Wakati,Fedha Za Masaa Ya Ziada  Ambapo  Wamefanikiwa  Kupunguza Vifo Vya Watoto Wachanga Na Watoto Chini Ya Miaka Mitano. 

Kwa Upande Wao Wauguzi Wakizungumza  Mara Baada Ya Hotuba Ya Mgeni Rasmi  Wametaka Serikali Kuwaboreshea Mazingira Ya Kufanyia Kazi   Kwaajili Ya Usalama Wao   Ambapo Wametolea Mfano Hospitali Ya Kibena Ambayo Mazingira Yake Yanahatarisha Usalaama Wao Kwa Kukosa Uzio  Na Kutaka Kupewa   Malipo Ya Masaa Ya Ziada  Pamoja Na Malipo Ya Likizo  Yatolewe Kabla Ya Kwenda Likizo.

Maadhimisho Ya Siku Ya Wauguzi   Duniani Kwa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Yamefanyikia Katika 

Hospitali Ya Kibena  Huku  Kwa Mkoa Wa Njombe Yakifanyikia Wilayani Makete Yakiwa Na Kauli Mbiu 

Isemayo  Wauguzi Ni Nguvu Ya Mabadiliko  Ya Uboreshaji  Wa Mifumo Ya Afya.














 MGENI RASMI BAADA YA KUSIMAMA KUTOA HOTUBA YAKE





 WAUGUZI WAKIPELEKA ZAWADI KWA WAUGUZI WANAOTARAJIA KUSTAAFU


 RISALA YA WAUGUZI IKIWASILISHWA KWA MGENI RASMI LEO KATIKA UKUMBI WA CHUO CHA WAUGUZI KIBENA


 WAUGUZI HAPA WANAONESHA FANI YA KUIGIZA KWA NKUTOA HUDUMA KWA WAGONJWA WAKIWA MBELE YA MGENI RASMI


HUU NDIYO UKUMBI WA CHUO CHA UUGUZI KIBENA




Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276