Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

MSAMBICHAKA LUDEWA AZINDUA RASMI KAMPENI UBUNGE BAADA YA GORI LA MKONO KUDAKWA

$
0
0
Na Erasto Mgeni Ludewa

Mara baada ya mgombea wa ubunge jimbo la ludewa kupitia chadema Bathromeo msambichaka  kushinda pingamizi aliyowekewa na mgombea ubunge kupitia chama cha mapinduzi  Deo Filikunjombe  mgombea huyo amezindua bkampeni za uchaguzi huku akiwahakikishia wananchi kushinda kwa kushindo

Msambichaka aliwekewa pingamizi na deo filikunjombe kwa madai ya kuwa alishindwa kurejesha fomu ya ubunge namba 10 sababu iliyomuondolea kigezo cha kuwa mgombea

Akiwa katika  mkutano ulifanyika katika viwanja vya sokoni mjini Ludewa amesema katika mchakato wa ujazaji fomu yeye alikamilisha kila kilichohitajika  na kuzirejesha  fomu hizo na alishangazwa na kitendo cha tume kumtangaza deo Filikunjombe kuwa amepita bila kupingwa hali iliyomfanya kukosa imani na tume ya uchaguzi

Miongoni mwa vipaumbele  vyake endapo wananchi watamchagua  ni pamoja na  swala la elimu,afya,miundombinu ya barabara na maji,uchumi wa mtu binafsi na pato la taifa

Hata hivyo msambichaka amewaomba wananchi kutoyumbishwa na wanasiasaa ambao wanatafuta madaraka na sio utumishi  bali wathamini haki yao ya kidemokrasia kwa kumchagua kiongozi wanae mtaka huku akiwaomba wananchi kuonyesha ushirikiano

Kwa upande wake Emmanuel Kayombo akizungumza kwa niaba ya katibu wa chadema mkoa wa Njombe Bwana Alatanga nyagawa amesema chadema imejipanga kushinda kwa kishindo uchaguzi huo kuanzia ngazi ya udiwani mpaka ikulu

Kayombo amewaomba wananchi kuelekeza kura zao kwa wagombea wa ukawa kwani umoja huo umedhamilia kuleta mabadiliko nchini Tanzania

Kastory nziku ni mwenyekiti wa chadema wialaya ya ludewa ameseam chama hicho kimewasimamisha madiwani katika kata zote 26 lakini karibu kata zote ziliwekewa pingamizi akidai kuwa ni hujuma zilizofanywa na chama cha mapinduzi kwa kuwachomolea wagombea hao fomu namba kumi na kwamba mpaka sasa wamekwisha kuawndika barua ya kuomba mkurugenzi wa uchaguzi aondolewe katika wilaya hiyo ili kuondokaba na hujuma zinazoweza kujitokeza wakati wa uchaguzi

Hali imekuwa tofauti na ramani iliyochoreka katika akili za wananchi  waliowengi zaidi kuwa hakuna mwamkoa mkubwa wa Chadema katika wilaya ya ludewa bali ukweli ni kwamba wananchi sasa wameamka na ktumia demokrasia yao kwa kujitokeza kwa wingi katika mkutano huo wa siasa kusikiliza sera ya mgombea wao



Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles