Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276
↧

Mwarobaini wa migogoro ya leseni za madini Kanda ya Kusini kupatikana.

$
0
0

1Afisa Madini Mkazi kutoka Nachingwea Mayigi Makolobela, akifungua mafunzo kuhusu huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini kutoka katika wilaya za Ruangwa, Liwale na Nachingwea mkoani Lindi.
2Sehemu ya washiriki wa mafunzo kuhusu huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini (hawapo pichani)
4Afisa Madini Mkazi kutoka Nachingwea Mayigi Makolobela, akielezea hali ya maombi ya leseni za madini katika wilaya ya Nachingwea katika mafunzo hayo. Kutoka kulia ni Charles Gombe na Upendo Elisha ambao ni wawezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
3 Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo akichangia mada kuhusu faida za huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao.
5Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Erick Mkoma akielezea mikakati ya Serikali katika ukusanyaji wa kodi za madini kwa kutumia mfumo wa huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactiona Portal; (OMCTP).
………………………………………………………………………
Na Greyson Mwase, Nachigwea
Imeelezwa kuwa dawa ya migogoro katika umiliki wa leseni za madini Kanda ya Kusini, itapatikana baada ya ofisi ya madini iliyopo Nachingwea kuanza kutumia huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao.Hayo yalisemwa na Afisa Madini Mkazi kutoka Nachingwea Mayigi Makolobela alipokuwa akifungua mafunzo kuhusu huduma ya leseni za madini kwa njia ya mtandao yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini katika wilaya za Ruangwa, Liwale na Nachingwea zilizopo mkoani Lindi.Makolobela alisema awali katika wilaya hizo kulikuwepo na migogoro ya umiliki wa leseni za madini iliyosababishwa na wamiliki wa leseni kuingiliana kwenye maeneo yao ya
kazi huku kila mmoja akidai ni mmiliki halali wa eneo husikaAlisema wakati mwingine, maombi ya leseni yalikuwa yanagongana kutokana na wamiliki tofauti kuomba eneo moja ambapo inapotokea aliyewahi kutuma maombi akapatiwa leseni, mwombaji anayefuatia hudai kuwa kuna upendeleo umefanyika.Alieleza kuwa katika mfumo huu mpya, mara baada ya maombi ya leseni kufanyiwa kazi kwa njia ya mtandao, mfumo hautaruhusu mwombaji mwingine kuomba leseni ya uchimbaji wa madini ya eneo husika.Alisisitiza kuwa mbali na kuondoa migogoro kwenye umiliki wa leseni za madini, mfumo huu utawezesha maombi mengi ya leseni za madini kufanyiwa kazi kwa haraka kwa kuwa maombi yote yatajazwa na waombaji wa leseni wenyewe.Wakati huohuo Makolobela alisisitiza waombaji wa leseni kufuata sheria na kanuni za madini wakati wa maombi na usimamizi wa leseni za utafutaji na uchimbaji wa madini.
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Latest Images

Trending Articles