Quantcast
Channel: GABRIEL KILAMLYA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Article 1

$
0
0

Waziri Mkuu Pinda afungua Mkutano wa mawaziri wa mazingira na mambo ya nje



 Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Peter Pinda (wa pili kulia waliokaa)akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka  Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika wakati wa ufunguzi wa mkutano huo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Peter Pinda( wa pili kulia waliokaa)akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi kutoka  Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka  Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la  kujadili changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi hizo leo jijini Dar es Salaam.( Picha na Lorietha Laurence-Maelezo)

 Kamishna wa Umoja wa Afrika anayeshughulikia Uchumi Vijijini na Kilimo Roda Tumusiime  akizungumza na wajumbe ambao ni Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika wakati wa ufunguzi wa mkutano huo jijini Dar es Salaam   kujadili changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi za Afrika. 
 Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Peter Pinda  ambaye pia ni mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika akisoma risala ya ufunguzi wa  mkutano huo jijini Dar es Salaam wenye lengo la kupata muongozo wa kujadili changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa nchi za Afrika ili kuwasilisha maazimio hayo katika mkutano unaotarajiwa kufanyika Septemba 23,2014 nchini Marekani.
 Wajumbe wa mkutano wa Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika wakifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo leo  jijini Dar es Salaam.

 Waziri wa Maji na Mazingira wa Uganda  Eprahim Kamuntu akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi leo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi rasmi wa mkutano wa siku moja wa Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika.
 Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Peter Pinda (katikati) ambaye pia ni mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa Mawaziri wa Mazingira na Mambo ya Nje kutoka Nchi za kamati ya Wakuu wa Nchi za Afrika  akifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo leo  jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Kamishna wa Umoja wa Afrikaanayeshughulika  Uchumi wa Vijijini na Kilimo Roda Tumusiime na kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais mazingira Dkt.Bilinilith Mahenge.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2276

Trending Articles